MAANA HALISI YA USHOGA WA KISIASA, OGOPA KAMA UKOMA, EPUKA KUTUMIKA

MAANA HALISI YA USHOGA KATIKA SIASA.

Wapendwa wasomaji wa makala zangu kwanza kabisa niaze kwa salamu, shikamoni wakubwa, habari za leo na hamjambo mlio wadogo kwangu. Ni tumaini langu mu wazima huku mkiendelea kushangilia umasikini tulionao. Awali ya yote ningependa kutoa ufafanuzi kidogo juu ya ushoga japo niliwahi kuandika andiko la kufanana na hili mwaka wa jana mwenzi wa kumi na moja, wengi walikimbilia kutukana tu bila kuangalia maudhui ya andiko nilichokiandiko ndicho kinachoendelea hivi sasa inshallah tuachane na hayo.

Nisikuchoshe usinichosha"Ushoga"una maana kuu mbili nijuavyo mm na wachache au wengi wetu.
Maana ya kwanza ushoga ni tabia ya mwanaume kuingiliwa kinyume cha maumbile na mwanaume mwenzake yaani mwanaume kuingizwa uume na mwanaume mwenzake kwenye tundu la kutolea haja kubwa (kinyesi) .

Hali hii humfanya mtu anayeingizwa kujikuta kuhitaji mara kwa mara kutokana na muwasho anaoupata siku chache baada ya tendo hilo chafu na ovu, kwani wadudu/bacteria  ambao wapo pale kwenye tundu wapo kwa ulinzi wa mwili  au eneo husika  na hutafuna mabaki ya pale tunduni(normal flora na ulizi wa eneo husika)  wanakuwa wameingiliwa na ugeni yaani chakula ambacho ni kitamu zaidi ya mabaki yaani  shahawa sasa.

Kutokana na utamu wa shahawa zile wale wadudu huvamia hata kwenye nyama ya puru au pale tunduni hali inayoongezea muwasho zaidi na zaidi.

Lakini kumbuka ushoga huu ni chukizo kwa Mungu,  ukipitia ktk kitabu cha Mambo ya Walawi 20:13 biblia inasema "Tena mtu mume akilala pamoja na  mtu mme kama alalavyo na mtu mke wote wawili wamefanya machukizo, hakika watauawa;damu yao itakuwa juu yao"  hata ukipitia kitabu cha walawi 18:22 vivyo hivyo Warumi 1:27 Pia vitabu vingine vingi katika vitabu vyote vitakatifu yaani Biblia na Quaran vinaonesha kuwa tendo hilo ni chukizo mbele za Mungu. Mwogope sana anayeshadadia au kupenda hayo hakika mkimbie na usikae jirani naye.

Maana ya pili ya Ushoga, ni neno ambalo wanawake wanapenda kulitumia ikiwa na maana rafiki, mtu wa karibu au mtu anayeshirikiana naye kwa mambo mbalimbali ikiwemo umbeya n. k
Utakuta mdada anasema "niambie shoga yangu" kwao ni neno la kawaida lakini si kwa mwanaume mwenzangu, ogopa sana hili neno.

Nitajikita zaidi zaidi ktk maana ya kwanza ya ya Ushoga, maana ya pili sitaitumia hapa nitaitumia makala ijayo.

Kwa maelezo hayo juu tuone nini maana ya ushoga katika siasa ambalo ndilo lengo kuu la makala hii.

Ushoga katika siasa ni hali ya mtu yeyote awe kijana au mzee, msomi au sio msomi mrefu au mfupi ambaye yupo tayari kusimama na kuwatetea wanasiasa kwa maslahi binafsi na si kwa maslahi ya kitaifa , kwa kifupi ni mtu kutumiwa na wanasiasa kwa maslahi binasi (anayetumika ni mfano wa mwanaume anayeingizwa uume, Pesa ni mfano wa Shahawa anayewatumia ni mfano wa mwanaume anayeingiza uume kwa mwanume mwenzake  na hawa wote ni chukizo mbele za Mungu). Naomba uelewe hivi kuna kutumiwa, kutumia na kuingia kwa ugeni unaotoka kwa mtumiaji (pesa/shahawa) ugeni huu humkuta anayetumiwa kama wewe kama ni mhusika , naomba kiswahili kilichotumika hapa kieleweke hivyo.

Kwa maelezo hayo jitathimini upo upande upi kama ni mhusika katika hili
Imekuwa ni jambo la kawaida kwa vijana hata wazee, wasomi nao kujikuta wanatumiwa na wanasiasa kwa lengo la kujipatia kipato ili kuendeleza familia zao lakini wanasahau kwamba wanaathiri maisha ya wa Tz wengine zaidi ya milion 40's

Inasikitisha sana kwa jamii inayotunguka kuona vijana wengi wanaojiita wasomi kwa asilimia kubwa wamejikuta wameangukia kwenye kundi hili la Mashoga wa kisiasa
Mbaya zaidi kuwatetea walewale waliotutengenezea mfumo huu unaotutafuna, ushoga ni kukubali na kuwa muumini wa siasa za kumwaga pesa ili kujinufaisha baadaye.

Haiwezekani kijana unayetaabika na kupigika ukakubali kutumiwa na wanasiasa hasa ndani ya chama tawala huku unaona hospitali hazina madawa, machinga wanataabika, maisha magumu, demokrasia inaminywa, walimu na mapolisi wanapigika hakuna cha mkulima wala mfanyakazi.
Mtu wa aina hiyo ni Shoga wa kisiasa naomba ieleweke hivyo ukikasirika ni ww mm nafikisha ujumbe tu na napenda ukasirike.

Lakini siwalaumu sana wanaokuwa mashoga wa kisiasa ni mfumo uliowaweka hivyo ni sawa na kurithi katabia ka wizi, watu hatujaelimika bali tumemeza madesa tu darasani na wengine tumepita kwa huruma ya tunaowashabikia na kujiita mara ooh mimi team EL, team BM, team MN, Team SW, team JM ooh sijui nani, huu ni ujinga usio na kifani Tujitathimini upya tuangalie haya tuyafanyayo yanamaslahi kwa taifa letu leo na baadaye BADIRIKA WW ACHA KUTUMIKA

Haiwezekani ndani ya miaka 50's ya uhuru bado tunazungumzia hali duni ya afya, hali duni ya maisha, elimu duni, miundo mbinu hovyo kila kitu hovyo lakini bado hao hao wahujumu uchumi waliokufanya ww ukose bumu, ukose elimu safi, ukose kila kitu kinzuri kwa sasa unashindwa hata kumnunulia mama yako kanga tu, chumvi tu halafu unawashabikia kwenye mitandao majizi, mafisadi, wahujumu uchumi eti ndio rais, hadharani huoni aibu, humuonei huruma nduguyo anayetaabika huko kijijini alaaaa

Hebu jiulize wamekuwa mawaziri katika serikali iliyotufikisha hapa palipo pabaya leo ww shoga wa kisiasa unakuja unaunga mkono danganya toto wanazozifanya ebooooooo ninahasira nisije kukupasua bure.

BADIRIKA KIJANA MWENZANGU ACHA USHOGA WA KISIASA HATA KAMA SHAHAWA (PESA)  ZA MWANAUME MWENZIO ZIMEKOLEA

Cybercrime usiniguse huu ni ufafanuzi tu wa maana halisi ya Ushoga wa siasa.

KILAWA THE IRON woga kwangu ni dhambiaa

Comments

Popular posts from this blog

KILIMO CHA NYANYA

Posho hii ifike hadi kwa walimu