Posts

Showing posts from April, 2016

UGONJWA WA KISUKARI UNAVYOPUNGUZA NGUVU ZA KIUME

Image
Ugonjwa wa kisukari (Diabetes Mellitus) huambatana na ongezeko la sukari(glucose) katika damu kwa kiwango kinachozidi kawaida. Homoni aina ya insulin ambayo hutolewa na kongosho ama hushindwa kufanya kazi yake vema kwa sababu ya kasoro za seli au hutolewa kwa kiasi kisicho kidhi uhitaji wa kuratibu sukari katika damu. Kwa hivyo sukari hubaki katika damu kwa wingi na kuleta madhara kadhaa.Wagonjwa wa kisukari pia huweza kuwa na kiwango kikubwa cha lehemu (cholesterol) katika damu. Na zaidi huweza kuwa na tatizo la mgandamizo wa damu (hypertension) au presha. Asilimia 55 ya wanaume wenye kisukari hupatwa na tatizo la nguvu za kiume. Mambo haya matatu, Sukari, lehemu (Cholesterol) na Mgandamizo wa damu, Huweza kusababisha upungufu wa nguvu za kiume.(Erection dysfunction). 1. Sukari. Sukari nyingi katika damu huweza kupelekea kuharibiwa kwa kuta za mishipa ya damu. Kisha kuta hizi hushindwa kuzalisha homoni aina ya Nitrogen Oxide ambayo husaidia kutanua mirija ya damu kwa ajili ya kupitish

MEYA WA KINONDONI AGAWA BURE MAENEO YA BIASHARA ASUBUHI YA LEO

Image
Meya akiongea na wafanyabiashara leo la asubuhi Meya wa Manispaa ya Kinondoni Mhe. Boniface Jacob leo Ijumaa 29/04/2016 amefanya ziara katika eneo la ubungo na kuongea na wafanyabiashara ikiwemo kuwaonyesha eneo la kufanya biashara zao. Amewataka wafanyabiashara hao kesho wasiwepo maeneo hayo na kuhamishia biashara zao katika eneo la soko la Mawasiliano (Sinza), kwani wasipofanya hivyo Kamati ya usalama na ulinzi  na usalama Manispaa ya Kinondoni imeshakaa na imepanga kuwaondoa. Meya ameona isingekuwa busara kuwaondoa bila kujua watakwenda wapi, Meya amewakabidhi wafanyabiashara hao kadi ambazo watazionyesha ili  wasisumbuliwe,pia amewataka wasilipe pesa yeyote endapo watatakiwa walipie maeneo ya biashara waliyopewa. Pia amesema kuhusu ushuru hawatalipa kwa muda wa mwezi mmoja baada ya hapo watalipia, amewahakikishia wafanyabiashara hao hakuna atakayekosa eneo la kufanya biashara. Afisa biashara wa Manispaa ya Kinondoni amewataka wafanyabiashara kutokaidi agizo hilo kw

WAAJIRI KATIKA TAASISI MBALIMBALI WILAYANI MTWARA WAMETAKIWA KULIPA WAFANYA KAZI WAO UJIRA KULINGANA NA KAZI WANAZO FANYA

Image
Wamiliki na waaajiri katika taasisi mbalimbali wilayani mtwara wametakiwa kuwajali na kuthamini michango ya wafanya kazi wao kwa kuangalia kazi wanazofanya na zilingane na mishahara wanayowapatia kwa mwezi. Akitoa wito huo katika mahafali ya wahitimu wa huduma za hotelini yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Old Boma mikindani mkuu wa wilaya mtwara Bi Fatuma Alli amesema kuwa wafanya kazi wengi katika hoteli zilizopo mjini mtwara hawalipwi ujira mkubwa kulingana na kazi wanazofanya na kupelekea kuwepo kwa vitendo visivyo vya kimaadili katika maeneo yao ya kazi. Bi Fatuma Alli amewataka wahitimu hao kuheshimu mikataba wanayopewa na waajiri wao kwa kuwa na nidhamu ,heshima,Busara na kuendana na maadili ya kitanzania wakiwa katika huduma zao kwa wateja na wafanya kazi wengine. Mkuu huyo wa wilaya pia amewataka wahitimu hao kujiendeleza kielimu ili kuendana soka la ajira la hivi sasa nchini na Dunia kwa ujumla,N a kuwashauri kama vijana kuwa tayari kukabiliana na mabadil

MAISHA NA UGONJWA WA KISUKARI

Image
Ugonjwa wa kisukari (Diabetes Mellitus) ni ugonjwa sugu unaotokea wakati fisiolojia ya mwili inaposhindwa kuratibu kiwango cha sukari katika damu. HIvyo sukari hupanda kwa kiasi kinachozidi kawaida na kusababisha matokeo hasi mbalimbali mwilini. Baadhi ya matokeo hasi yanayoletwa na kisukari ni Kupatwa na mgandamizo wa damu (presha), Upofu unaosababishwa na kuharibika kwa Retina ya jicho (retinopathy), magonjwa ya figo (nephropathy), magonjwa ya neva za fahamu (neuropathy), Kuharibika kwa mirija ya damu (diabetic angiopathy) nk. Magonjwa ya neva za fahamu na mirija ya damu huweza kusababisha vidonda sugu visivyopona na kupelekea ulazima wa kukatwa mguu au mkono kutegemea na eneo kilipo kidonda. Kwa hiyo moja kati ya changamoto kubwa kwa mgonjwa wa kisukari ni kuepuka majeraha. Njia mbali mbali zaweza kusaidia kuepuka matokeo hasi ya ugonjwa wa kisukari. 1. Kuacha kabisa kuvuta sigara. 2. Kufanya mazoezi mepesi (aerobic exercise) ili kuchangamsha mzunguko wa damu. 3.Kupunguza ku

LEICESTER CITY KUITIA HASARA KAMPUNI YA KAMALI

Image
Timu LEICESTER CITY wakishangilia goli katika moja ya mechi zao. Kushoto chini ni Washambuliaji, Vardya na Mahrez. Kulia ni Leigh Hebert, mashabiki anayesubiri kushinda kitita cha Pauni 25,000 endapo timu yake ya LEICESTER CITY itabeba ubingwa wa ligi kuu msimu huu.                                                           Mazoezi ya LEICESTER CITY. Endapo LEICESTER CITY itashinda kombe la ligi kuu Uingereza msimu huu, basi fundi seremala kutoka kitongoji cha Guildford huko Uingereza atashinda kiasi cha pound 25,000, zaidi ya Tsh milioni 75 baada ya kuweka 'bid' ya paund 5 (Tsh. Elfu 15) kwenye mchezo wa kamali; Fundi Leigh Hebert, amekataa ofa ya paund 3200 (Tsh milioni 9.6) aliyopewa na kampuni hiyo ya kamali ili aondoe utabiri wake na kusema anataka kushinda paund zote 25000 au hata akipoteza paund 5 aliyoweka haina noma. "Nataka kushinda kiasi cha paund 25,000 nitumie na mchumba wangu KERRY, nimechoka kuishi nyumba za kupanga" anasema Leigh Hebert mw

SUKARI: MTIHANI WA KWANZA SERIKALI YA MAGUFULI KUFELI.!

SUKARI: MTIHANI WA KWANZA SERIKALI YA MAGUFULI KUFELI.! By Malisa GJ, Takribali Miezi miwili iliyopita Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr.John Pombe Magufuli alipiga marufuku uingizwaji wa sukari nchini kwa madai ya kusaidia kulinda viwanda vya ndani vinavyozalisha biidhaa hiyo nchini. Rais Magufuli alitoa agizo hilo wakati akizungumza na wafanyabiashara ambapo alitaka agizo hilo lianze kutekelezwa mara moja. Baada ya utekelezaji wa agizo hilo kuanza kumejitokeza mfumuko mkubwa wa bei katika bidhaa ya sukari ambayo imepanda kutoka Shilingi 1,800/= kwa kilo moja hadi shilingi 2500/- huku baadhi ya maeneo ikifika shilingi 2800/-. Ongezeko hili ni wastani wa asilimia 39% hadi 55% kwa kilo moja ya sukari. Yani mfumuko wa bei ya sukari umefikia asilimia 55% ndani ya kipindi kisichiozidi miezi miwili. Hii ni ishara mbaya sana kiuchumui (Indicator for galloping inflation). #Kwanini_Rais_alizuia_sukari_kutoka_nje? Rais Magufuli alipiga marufuku uingizwaji wa sukari ya nje ili

ALIYEVUMBUA 'TAFADHALI NIPIGIE' AISHINDA VODACOM MAHAKAMANI

Image
Ni NKOSANA MAKATE, kijana aliyegundua huduma ya tafadhali nipigie akiwa mfanyakazi wa Vodacom huko Johannesburg nchini Africa kusini. Hiyo ilikuwa Nov 2000.  Ilipofika February mwaka 2001 huduma hiyo ilianza kutumiwa rasmi na Vodacom. Hata hivyo Mr. Makate alitaka kulipwa fedha kwa uvumbuzi wake huo ambao umeingizia Vodacom faida ya dola za kimarekani bilioni tano. (USD 5b). Ndipo alipofungua kesi mahakamani baada ya 'kudhurumiwa' haki yake.  Mwaka 2014, Mahakama ya mjini Johannesburg iliipa ushindi kampuni ya Vodacom kwa kigezo kwamba Mr. Makate alikubaliana kwa maneno na Mr. Phillip Geissler ambaye alikuwa mkurugenzi wa maboresho ya huduma za kampuni. Mahakama ilisema kwamba Mr. Makate na Mr. Geissler walikubaliana kwa maneno na hivyo kampuni ya Vodacom haihusiki.  Lakini tar. 26/04/2016 mahakama ya katiba nchini Africa kusini imeamua kuwa Vodacom imlipe Mr. Makate ndani ya siku 30. Haijajulikana Mr. Makate atalipwa kiasi gani ingawa mwenyewe alitaka kulipwa asilimi

TAIFA STARS KUJIPIMA NA KENYA MEI 29

Image
Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars), inatarajiwa kucheza mchezo wa kirafiki wa kimataifa na timu ya Taifa Kenya (Harambee Stars) Mei 29, 2016 jijini Nairobi. Mchezo huo wa kirafiki utachezwa jijini Nairobi Mei, 29 mwaka huu, ikiwa ni sehemu ya maandalizi kwa timu zote mbili kujaindaa na michezo ya kuwania kufuzu kwa Fainali za Mataifa ya Afrika mapema mwezi Juni, 2016. TFF kwa kushirkiana na FKF zimekubaliana kuwepo kwa mchezo huo wa kirafiki, utakotumika kama sehemu za maandalizi kwa timu zote kujiandaa na michezo ya kuwania kufuzu kwa AFCON 2017 mwezi Juni. Kikosi cha Taifa Stars kianchonolewa na kocha mkuu, Charles Boniface Mkwasa kinatarajiwa kuingia kambini mwezi Mei, mara baada ya kumalizika kwa ligi kuu ya Vodacom (VPL) kujiandaa na mchezo huo wa kirafiki kabla ya kuwakabili Misri katika uwanja wa Taifa jijini Dra es salaam Juni 04, 2016. Stars inajianda na mchezo wa kuwania kufuzu kwa Fainali za Mataifa Afrika mwaka 2017 nchini Gabon dhdi ya Misri utakaochezwa

HATARI YA KUTOA MIMBA PASI NA UTAALAMU.

Image
Wasichana wengi hujikuta wakipata ujauzito bila kupanga. Kwa hiyo hupatwa na mawazo ya kutoa ujauzito huo bila ya kupima faida na hasara za kuutoa. Hata hivyo pamoja na kuwa hairuhusiwi kisheria kutoa mimba (abortion) ambayo haina hatari kwa afya ya mama,lakini ikilazimika, basi utoaji mimba ufanyike katika mazingira salama,ambayo ni nadra kupatikana hasa katika mataifa machanga na ambayo yanapiga marufuku utoaji mimba. Zifuatazo ni hatari zinazoweza kutokea wakati na/au baada ya kutoa Mimba. 1. Kutokwa damu nyingi,(Haemorrage) mfuko wa mimba una mirija mingi ya damu mahususi kwa ajili ya kuhudumia kijacho kwa hewa na virutubisho. Utoaji mimba huweza kupelekea kupasuka kwa mirija hiyo midogo kwa mikubwa kisha kuvuja na kusababisha upungufu mkubwa wa damu wa ghafla (Shock) au hata kifo. 2.Kutoboka kwa mfuko wa mimba (uterine wall perforation). Ikiwa utaalam hautakidhi au kwa bahati mbaya, vifaa vitumikavyo katika utoaji vyaweza kutoboa mfuko wa mimba na pia kuharibu ogani za karibu y

RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO TANZANIA DR JOHN POMBE MAGUFULI ATEUA MAKATIBU TAWALA WA MIKOA 26 YA TANZANIA BARA

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 25 Aprili, 2016 amefanya uteuzi wa Makatibu Tawala wa Mikoa 26 ya Tanzania Bara. Taarifa iliyotolewa leo na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa kati ya Makatibu tawala hao 10 ni wapya, 2 wamebadilishiwa vituo vya kazi na 13 wamebakisha katika vituo vyao vya sasa. Makatibu Tawala wapya walioteuliwa ni kama ifuatavyo;     1.Arusha -    Richard Kwitega     2.Geita -      Selestine Muhochi Gesimba     3.Kagera -     Armatus C. Msole     4.Kilimanjaro -     Eng. Aisha Amour     5.Pwani -      Zuberi Mhina Samataba     6.Shinyanga -   Albert Gabriel Msovela     7.Singida -     Dr. Angelina Mageni Lutambi     8.Simiyu -    Jumanne Abdallah Sagini     9.Tabora -   Dkt. Thea Medard Ntara    10.Tanga -    Eng. Zena Said Makatibu Tawala waliobadilishwa vituo vya kazi ni kama ifuatavyo; 1.Kigoma -   Charles Amos Pallangyo (Kutoka Mkoa wa Geita) 2.Morogoro -  Dkt. John

KWANINI SERIKALI YA AWAMU YA TANO CHINI YA DR JOHN POMBE MAGUFULI IMEZUIA BUNGE KUONESHWA MOJA KWA MOJA YAANI LIVE?

Image
Mh Freeman Mbowe akiongea na vyombo vya habari  Na Kilawa the Iron Ndugu zangu watanzania najua  wengi wetu hatujui kuwa tumewekwa katika dimbwi lililojaa uchafu wa kila aina ilihali aliyetuweka katika dimbwi hilo  akitudanganyishia asali kwa muonekano wa nje na wananchi wengi tumeamini kuwa tupo kwenye dimbwi lilojaa  asali la hasha. Hivi ni kweli sisi sote takribani watu karibu milioni hamsini hatuoni kuwa tupo katika lindi la giza nene ambalo linaweza kuathiri kuona kwetu kuwaza na kuwazua kwetu na fikra zetu ? Hivi ni kweli kwamba sisi sote hatujui kusoma na hata picha tu hatuoni? Haiwezekani. Japo wahenga walisema mwenye macho haambiwi ona lakini mm nadhani  ni bora na ni vyema nikakutonya Mtanzania mwenzangu ili uone tu, maana haya yanayoendelea yataathiri kizazi hiki na kijacho tena kwa kasi ya mlipuko wa ebola, dengue au kipindupindu. Hata hivyo kwanini usione ndugu yangu  wakati tunaambiwa macho hayana pazia? Funguka chukua hatua. Ukilinganisha kwa haraka hara

SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF) YATANGAZA LIGI KUU YA MIKOA KUAZA KUTIMUA VUMBI HIVI KARIBUNI

Image
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limetangaza Mei 14, 2016 kuwa tarehe ya kuanza kwa Ligi ya Mabingwa wa mikoa (RCL) itakayozishirkisha bingwa wa kila mkoa kutoka katika mikoa 27 nchini. Ligi hiyo ya mabingwa wa mikoa itachezwa katika vituo vine nchini, ambapo mshindi wa kila kundi atapanda moja kwa moja ligi daraja la pili (SDL) na mshindi wa pili mwenye matokeo mazuri kutoka kundi A, B na C. Kundi A kituo cha (Njombe) kutakua na mabingwa wa mikoa ya Ruvuma, Iringa, Mbeya, Rukwa, Katavi, Dar es salaam 3, Morogoro, Kundi B kituo cha (Morogoro) kitakua na mabingwa wa mikoa ya Pwani, Mtwara, Lindi, Dar es salaam 1, Dar es salaam 2, Tanga, na Singida. Kundi C kituo cha (Singida) kitakua na mabingwa wa mikoa ya Dodoma, Arusha, Kilimanjaro, Tabora, Kagera, Manyara, na Njombe, huku kundi D kituo cha (Kagera) kikiwa mabingwa wa mikao ya Geita, Mwanza, Shinyanga, Simiyu, Mara na Kigoma.

TFF YATANGAZA RASMI KUAZA KWA LIGI NDOGO

Kamati ya Mashindano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetangaza kuanza kwa ligi ndogo Mei 11, 2016 katika uwanja wa Karume jijini Dar es salaam itakayozishirikisha jumla ya timu nne. Timu zilishoshika nafasi ya pili katika msimamo wa SDL kwa kila kundi, Abajalo FC (Dar es salaam), Pamba FC (Mwanza), Mvuvumwa (Kigoma), Mighty Elephant (Songea) zitacheza ligi hiyo kusaka timu mbili zitakazoungana na timu nne za juu kupanda ligi daraja la kwanza (FDL) msimu ujao. Klabu nne za Allicane Schools (Mwanza), Mshikamano FC (Dar es salaam), Mbeya Warriors (Mbeya) na Singida United (Singida) zilizoongoza msimamo wa makundi ya SDL zitaungana na timu mbili kupanda ligi daraja la kwanza msimu ujao.

CHAMA CHA SOKA MTWARA, MTWAREFA CHATANGAZA TAREHE YA UCHAGUZI

Image
Kamati ya uchaguzi ya Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Mtwara (MTWAREFA), imetangaza tarehe ya kufanya uchaguzi na kuahidi kutenda haki na kufuata kanuni na sheria zilizopo katika katiba ya chama hicho na vyama vingine vya juu, ili mchakato wa uchaguzi ulioanza juzi umalizike kwa amanai na salama. kulia mwenye wa kamati ya uchaguzi MTWAREFA Husein King na mjumbe wa kamati ya uchaguzi Selemani Kachele Akizungumza na waandishi wa habari juzi katika ofisi za Mtwarefa, mwenyekiti wa kamati hiyo, Hussein Kingi, alisema kuwa kamati itahakikisha inafuata yale yaliyoelekezwa kwenye katiba na kanuni za uchaguzi na kwamba kitendeo cha kukiuka hayo ni kukaribisha malalamiko kutoka kwa wagombea yatakayopelekea watu kukata rufaa na kuweka mapingamizi hali ambayo wao kama kamati hawahitaji kitu kma hicho kujitokeza, ‘’sisi tunaahidi kutenda haki kwa kufuata kanuni zilizopo hatutaangalia huyu ni nani na anatoka wapi’’alisema mwenye wa kamati hiyo Husein King, na kusistiza kwamba hatutakwen

WANACHUO 33 KATI YA 36 WA CHUO CHA UALIMU MONTESSORI MTWARA WAFANYA MAHAFALI

Image
Wazazi  wametakiwa kutumia fursa iliyopo katika m koa  wa Mtwara kwa kutumia vyuo vilivyopo kuwapeleka vijana wao kupata elimu na taaluma mbalimbali zitolewazo kwenye vyuo hivyo. Akizungumza katika mahafali ya ya tano ya chuo cha ualimu Montessori kwa niaba ya mkuu wa mkoa  Mtwara ,mkuu wa wilaya Mtwara Bi Fatuma Ali amewataka wazazi kutumia fursa hii adhimu iliyopo katika mkoa wa huo kwa kuwapeleka vijana wao kupata elimu na taaluma mbambali zitolewazo kwenye vyuo hivyo ili kupunguza wimbi kubwa la vijana wanao zulula mitaani pasipo kazi maalum. Pia Bi Fatuma Alli amewashauri wahitimu hao kuwa tayari kukabiliana na changamoto mbali mbali watakazo kabiliananazo pindi watakapokuwa mtaani wakisubiria nafasi za ajira kutoka serikalini na kuwataka kufanya kazi popote pale watakapo pangiwa na serikali na kuachana na tabia zilizopitwa na wakati za kutaka kufanya kazi kwa maeneo mjini. Naye mwakilishi wa Afisa elimu mkoa Bi Jane Lutego ambaye pia ni afisa elimu watu wazima mkoa a

BREAKING NEWS : WABUNGE WA KAMBI RASMI YA UPINZANI WASUSIA BUNGE NA KUTOKA NJE

Image
            Wabunge wa kambi rasmi ya upinzani, watoka nje ya ukumbi wa bunge,,wakisusia kujadili bajeti ya waziri mkuu leo hii jioni wakizungumza na mwandishi wegu wabunge hao wametoa sababu kuu mbili Sababu ya kwanza ikiwa ni hakuna mwongozo wa kuendesha serikali mpaka sasa, inasemekan hadi hii leo wanatumia muongozo uliotumika na serikali iliyopita. Sababu ya pili ni kwamba wanahoji kwanini wanahabari waziiwe kuingia bungeni Endelea kufuatilia hapa tutazidi kukujuza kadri ya tutakavyopata habari

HOTUBA YA KIONGOZI WA UPINZANI BUNGENI (KUB) MHESHIMIWA FREEMAN AIKAELI MBOWE (MB) AKIWASILISHA BUNGENI MAONI YA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KATIKA OFISI YA WAZIRI MKUU KWA MWAKA WA FEDHA 2016/17

Image
Pichani ni Mh Freeman Aikael Mbowe - mbunge wa jimbo  hai kwa ticketi ya CHADEMA ,kiongozi mku wa kambi rasmi ya upinzani bungeni  Inatolewa chini ya Kanuni ya 99(9) ya Kanuni za Kudumu za Bunge, Toleo la Januari, 2016 _________________________________ 1. SHERIA YA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU YA MAWAZIRI (MINISTERS – DISCHARGE OF MINISTERIAL FUNCTIONS – ACT, 1980. Mheshimiwa Spika, kifungu cha 5(1) kinaweka masharti kwa Rais kutengeneza mwongozo wa muundo na utekelezaji wa majukumu ya Serikali yake. Inasomeka ifuatavyo: Nanukuu “the President shall from time to time by notice published in the Gazette, specify the departments, business and other matters and responsibility for which he has retained for himself or he has assigned under his direction to any minister and may in that notice specify the effective date of the assumption of that responsibility…….” mwisho wa kunukuu. Mheshimiwa Spika, mpaka sasa Serikali inafanya kazi bila kuwa na mwongozo wa utendaji wake na kazi kwa

JPM TUPIA JICHO MFUMO WA ELIMU NCHINI, NI "JIPU" KUBWA ZAIDI YA UDHANIAVYO.!

By Malisa GJ, Kati ya vitu navyotamani sana kuona vikifanyika ni marekebisho makubwa ya mfumo wa Elimu Nchini. Natamani kuona shule za sekondari za serikali zikirudishwa ktk hadhi yake. "Special schools" ziwe "Special" kweli. Tuone watoto wetu wakipambana kwenda Ilboru, Kibaha, Tabora boys, Mzumbe etc. Sio kupambana kwenda St.Marry's au St.Francis. Nakumbuka miaka 21 iliyopita kaka yetu alifaulu darasa la 7 kwenda sekondari ya Iyunga (Mbeya) akitokea kule kijijini Old Moshi. Wakati tunamsindikiza kupanda basi alikua anatupa hamasa ya kusoma ili tufanye vizuri zaidi yake. Kipimo kilikua kwenda "special school". Nakumbuka matokeo ya darasa la 7 au kidato cha 4 yalikua yakitoka tunaenda kujazana ofisi za Halmashauri ya wilaya kuangalia umepangwa wapi. Ruvu, Kigonsera, Kantalamba, Ndanda, Pugu, Magamba, Mwenge, Same, Mazengo au Mzumbe? KWA WAVULANA: Tabora boys, Songea Boys, Bwiru boys, Nsumba, Lyamungo, Umbwe etc. KWA WASICHANA: Weruweru, Ashi

MSTAHIKI MEYA WA MANISPAA YA KINONDONI MH BONIFACE JACOB AENDELEA KUCHANJA MBUGA KWA KASI YA AJABU ZAIDI YA MWENDO WA ROCKETI

Image
 Mh Boniface Jacob akiwa na wananch wake wakati akiendelea na ziara yake ya kuwagawia hundi za mikopo wananchi waliojiunga katika vikundi mbalimbali vya ujasiliamali. Hapo  kama unavyoana wananchi walivyofurahi kwa pamoja na mh wao, kushoto kwa mh ni kijana wa ccm akiwa na furaha kubwa sana kutembelewa na meya wake wa kinondoni Na kilawa the Iron Diwani wa kata ya Ubungo ambaye ni mstahiki meya wa manispaa ya kinondoni wa sasa Mh Boniface Jacob ameonekana kuwa na kasi ya ajabu katika utendaji wake  wa kazi ya kuwatumikia wananchi wa manispaa ya kinondoni amedhihirisha kuwa ni kiongozi wa mfano  wa kuigwa. Toka alipoaza kuwatumikia wananchi wa manispaa hiyo ya kinondoni amekuwa akifanya kwa vitendo na si kwa maneno au blabla. Ni imani yangu kuwa kama mameya wa manispaa nyingine zote nchini na wenyeviti wa halmashauri zote na viongozi wengine waliopewa mamlaka ya kuongoza wananchi wakiamua kufuata nyayo za Mh. Boniface Jacob basi tutaishi kama wafalme nchini hapa. Kwa kasi h

MADIWANI WAITAKA SERIKALI KUKARABATI BARABARA ZIENDAZO PEMBEZONI MWA MJI

Image
madiwani wakifuatilia kwa makini barala la utekelezaji bajeti Madiwani wameitaka halmashauari kupitia idara husika kuziangalia na kuzifanyia utaratibu wa kujenga  Barabara zinazo elekea pembezoni mwa mji ili kurahisisha hali ya usafiri kwa wananchi waishio maeneo hayo. Wakichangia agenda ya utekelezaji wa miundombinu ya barabara katika kikaoa cha baraza la madiwani kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya mtwara manispaa madiwani hao wameitaka Halmashuri na idara husika kuziangalia bara bara hizo kwa jicho la tatu kwani zinamchango mkubwa katika kuiingizia kipato  halmashauri hiyo. Madawani hao wakiongozwa Mh Masoud Dalli,Sharifa Ndille na Mh Bandali wamezitaja barabara hizo kuwa Barabara ya Mtwara kuelekea Naliendele moma,mkangala,Mdenga,likombe hadi ziwani,kijiji cha mbae sehemu ambayo hutoa mchango mkubwa wa mchanaga unaotumiwa ujenzi wa nyumba nyingi katika manispaa ya mtwara mikindani,pia ndio barabara zituwazo kuletea nishati ya kupikia kamavile kun

UPATIKANAJI AJIRA KIWANDA CHA CEMENT MTWARA CHA KUTWA NA KASHIFA NZITO

Image
Wananchi na viongozi wa vijiji vinavyo zunguka kiwanda cha cement cha DANGOTE mkoani mtwara wamewalalamikia wajiri   wa kiwanda hicho kuwepo kwa upendeleo na harufu ya rushwa katika upatikanaji wa   ajira kiwandani hapo. mwonekano wa nje wa kiwanda cha Dangote Akizungumza kwa hisia kali katiak kiakao kilichofanyika kwenye ukumbi wa shule ya msingi msijute mwenyekiti wa kijiji cha Naumbu kusini Bwa Hamza Fuja amesema kuwa matakwa na utaratibu ambao wao walipewa na mmiliki wa kiwanda hicho mwanzoni wakati kinajengwa imekuwa tofauti na utaratibu unafanywa hivi sasa’’ siku ya ufunguzi wa wa ujenzi wa kiwanda hicho Mh Alhaji Aliko Dangote alisema kuwa vijana na wananchi wa eneo linalozunguka kiwanda watapewa kipaumbele kwa nafasi za ajira lakini sasa hivi imekuwa tofauti na kauli hiyo’’. Mwenyekiti huyo amesema kuwa taratibu na matangazo ya ajira umekuwa usio ridhisha kwani hutoa matangazo ya kazi siku moja kabla ya usaili hali ambayo viongozi,vijana na wazee wa maeneo hus