Posts

Showing posts from July, 2015

MALEZI YA MTOTO, DEMOKRASIA NA HATIMA YA MAENDELEO YA NCHI YETU.

Image
Na Dr. Elias Mwakapimba Katika malezi ya mtoto kuna vitu vingi ambavyo vinaathiri afya kwa ukuaji mzuri. Vitu hivi ni elemu/uelewa wa mzazi, uwezo wao wa kiuchumi/kipato na mazingira wanamoishi. Haya mambo ni nguzo muhimu katika kuimarisha afya thabiti kwa ukuaji na mafanikio ya mtoto baadaye. Wazazi wa mtoto wanaweza kuwa na elimu/uelewa wa kulea mtoto lakini hawana uwezo wa kumudu mahitaji kwa afya njema ya mtoto. Wanaweza wakawa na kipato kizuri lakini wasiwe na elimu/uelewa wa namna ya kuanda lishe nzuri ya mtoto. Au wanaweza wakawa navyo vyote lakini mazingira yasiwe rafiki katika kuandaa lishe ambayo ni muhimu kwa afya ya mtoto (mfano vita/ukimbizi) au wakaweza kuandaa lishe lakini mazingira tena yasiwe rafiki kuruhusu mtoto kufaidi virutubisho vya lishe na asiweze kukua katika afya (mfano magonjwa). Katika makundi mawili ya awali: ukosefu wa elimu au kipato, au ukosefu wa vyote au uwepo wa vyote lakini mazingira yasiwe rafiki hupelekea mtoto kuwa na utapia mlo (mtoto

TATIZO LABDA NI MWALIMU NYERERE NA CCM YAKE.

Image
Na Mwl Bongole Tunapoelekea kwenye uchaguzi mkuu  Yapo mambo muhimu mengi na muhimu sana yanayopaswa kuzingatiwa na kuangalia kama kweli leo hii tunahitaji kukomesha ufisadi rushwa kuongeza fursa za ajira na kutoa huduma za jamii kwa kiwango ambacho kinaweza kukidhi haja ya watanzania. Ili kufikia mabadiliko ya kimfumo ambayo kiuhalisia chanzo chake ni kupoteza dira kwa chama cha mapinduzi basi tunahitaji mtu imara, jasiri, mwelewa, mwenye malengo na uzoefu wa kubadilisha mifumo iliyomibovu na kuleta mfumo mzuri. Kwa hapa tulipofikia ni vigumu sana yeyote ndani ya ccm kufumua mfumo uliozeeka wa kifisadi kibaguzi kandamizi na usiopenda mabadiliko. Mfumo uliopo ndani ya ccm umejikita katika kuangalia kulinda na kutetea CHAMA KWANZA huku vipaumbele kama afya elimu na aina zote za huduma za jamii zikiwa duni. Ni mfumo wa kutizama maslahi ya vyombo vya ulinzi kama vile Polisi kwa kuwekeza nguvu kubwa huko ili kuendelea kulitumia katika kufanikisha maslahi yake. Si jambo la aja

HAKUNA MATARAJIO MAPYA KWENYE MFUMO ULE ULE

Image
Na Musa Makongoro Tayari chama cha mapinduzi kimempata, mgombea urais wa chama hicho kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 kwa njia za mizengwe na kupelekea mpasuko ndani ya chama hicho kuonekana hadharani. Mgombea huyu ni Dr John Pombe Maghufuli, ambaye ni waziri wa ujenzi wa serikali inayoondoka madarakani. Ni kama vile watanzania wengi, wanakubali kwamba huyu ndiye anaeweza kuirudisha nchi pale ilipokuwa na kwamba atakidhi matarajio yao. Pamoja na umahili wake wa kukariri takwimu mbalimbali, kitendo kilichomjengea umaarufu miongoni mwa watanzania wengi wasiofuatilia mambo, John Pombe Magufuri ataingia kusimamia mfumo ule ule. Tumesahau kwamba ni Magufuri huyuhuyu, ameshiriki kupitisha sheria mbovu kabisa na zenye maslahi binafsi ya baadhi ya wana CCM bungeni. Wakati bunge maalumu la katiba likiizika rasimu ya jaji waryoba, iliyokuwa imesheni maoni ya wananchi alikuwamo bungeni na hakuonyesha nia yoyote ya kutetea wananchi wa Tanzania. Rundo la kashfa zikiwemo za upotevu wa m

JOHN POMBE MAGHUFULI AIBUKA KIDEDEA KWA 87.1%

Image
Ni saa 12:49  Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi (CCM), Dr Kikwete alipoanza kutangaza rasmi na kumuomba Spika wa Bunge aje mbele na kutangaza matokeo ya nani atapeperusha Bendera. Kwa maelezo ya Dr Kikwete alisema kura hizo zilihesabiwa na Spika wa bunge Anna Makinda wakishirikiana na Spika wa Zanzibar bwana Kificho  na wengine aliwataja, Anna Makinda ndiye alipewa fursa na Mwenyekiti wa CCM kutangaza rasmi matokeo hayo. Anna makinda aliaza kwa furaha na bashasha huku akipiga vijembe upande wa pili Aidha alimsifia Rais JK kwa kukamirisha ukumbi wao wa CCM  na mambo mengine aliyoyafanya. Pia hakusita kuwapongeza wanawake waliojitokeza kuwania nafasi ya urais wa Tanzania kwa ticket ya ccm.Alisema" kwa wanawake kugombea nafasi ya juu haijawahi kutokea, lakini Awamu ya nne imetokea" Alitaja matokeo kama  ifuatavyo Jumla ya kura zilizopigwa ni 2422, zilizoharibika ni kura 6. Asha  Rose Migiro  alipata kura 59 sawa na 2.4% Amina Salumu alipata kura 253   sawa na  

HAYA NI MATOKEO RASMI DR JOHN POMBE MAGHUFULI AIBUKA KIDEDEA KWA ASILIMIA KUBWA.

SOMA HAPA Jumla ya kura zilizopigwa ni 2422, zilizoharibika ni kura 6. Asha  Rose Migiro  alipata kura 59 sawa na 2.4% Amina Salumu alipata kura 253   sawa na  10.5% Na Dr. John Pombe Maghufuli alipata kura 2104 sawa  87.1%  Huyu ndiye atakayepeperusha bendera ya CHAMA CHA MAPINDUZI.

TANO BORA YA CCM IMEZUA MASWALI MENGI JUU YA WALIOZUNGUMZA WANAZUONI KABLA YA MCHAKATO WA KUPATA TANO BORA

Image
HAYAWI HAYAWI SASA YAMEKUA NDANI YA CCM, Hii ndo tano bora ndani ya CCM Wahenga walisema "Lisemwalo lipo na kama halipo lipo linakuja" usemi huu umejidhihirisha wazi baada ya kamati kuu kutoa tano bora. Kulikuwa na minong'ono ya mda mrefu kuwa Mh Bernad  Membe ndiye atakayekuwa mrithi wa Mh Dr. J. M. Kikwete na sababu kuu iliyotelewa ni kwamba inasemekana wawili hawa ni ndugu wa damu japo Mh Bernard  Membe alikanusha undugu wao hawa wawili na hakika halijathibitishwa kisayansi kama ni ndugu au la? Sasa swali linajirudia je ni kweli huyu ni chagua la J. K Kama wachambuzi wa siasa walivyosema mwanzo na mara zote waliyasema hayo,?  tusubiri  Tatu bora tutajua kama nani ni nani?  ila akishinda ningetamani kipimo cha DNA kifanyike kwa uwazi kutotoa hofu ya kurithishana uongozi watu wa familia moja (ndugu wa damu) huku kuna watu makini zaidi Kwa upande mwingine ilisemekana kuwa Mh Lowassa hatafika tano bora na hili pia limetimia na sababu kuu ilikuwa ni magovi ka
Image
RAIS WA JAMUHURI YA MUUNGANO AMEWATEUWA WASAIDIZI WAWILI Rais wa Jamuhuri ya Muungano Tanzania mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amewateua wasaidizi wake wawili. Uteuzi huo unaanza mara moja. Katika uteuzi huo, Rais Kikwete amemteua Bwana Jumaa George Bwando kuwa Mnikulu. Bwana Bwando ni mtumishi wa miaka mingi wa Serikali. Rais pia amemteua Bwana Martine Shigela kuwa Msaidizi wa Rais (siasa). Bwana Shigela anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Bwana Rajab Luhwavi ambaye karibuni aliteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara)
Image
MKAZI MMOJA ALALA JUU YA DARI KWAZAIDI YA MIEZI NANE MKOANI MTWARA Na Ernest Hyera MKAZI mmoja wa manispaa ya Mikindani mkoa mtwara amekuwa akilala juu ya dari kwa zaidi ya miezi nane sasa kutokana na nyumba yake kukumbwa na mafuriko kila mwaka. Pichani ni nyumba ambayo bi Zainabu anekuwa akilala juu ya dari ili kukwepa mafuriko kipindi cha mvua Akizungumnza na mwandishi wa blog hii Bi zainabu Musa Lipuga amesema toka mwaka jana mwezi wa kumi na moja amekuwa akilala juu ya dari kutokana na mvua iliyokuwa inanyesha na kubomoa sehemu ya chini ya nyumba anayoishi. Amesema hadi kufikia sasa hajamuona kiongozi yeyote waserikali ambaye ametoa msaada kwake zaidi ya vyama vya siasa vya upinzani ambao walifika na kumsaidia. Bi Zainabu amesema kwa sasa Chama Cha Wananchi CUF ndio walifika hapo na kumjengea chumba kimoja kilicho gharimu zaidi ya milion 2, kwa ajili ya kuishi kwamuda. Pichani ni ni ujenzi wachumba ambacho Cha Wananchi CUF wamemjengia bi Zainabu Kwa upande wa Ch

HALI BADO NI TETE KUMPATA MGOMBEA ATAKAYEPEPERUSHA BENDERA YA CCM

Image
Mapigo ya moyo yanakwenda kwa kasi sana ,si mchezo Habari kutoka mjini Dodoma baada ya  Nape Nnauye katibu wa itikadi na uenezi wa chama cha mapinduzi (CCM) kuongea na waandishi wa habari ,anasema vikao vyote vitakaa leo kuanzia SAA 4:00 Asubuhi ili kumpata atakayepeperusha bendera ya chama chao,aidha amesema baada ya kamati kuu kutoa tano bora majina yatepelekwa kwenye kamati ya mashauriano na taratibu nyingine zitafuata. Endelea kufuatilia kujua kinachojili huko