Posts

Showing posts from 2017

Uhakiki unatumika kuminya haki za watumishi wa umma!

NA RUSTON MSANGI. Mapema mwezi  Aprili na Mei 2017, serikali ilitangaza hadharani idadi ya watumishi wa umma wenye vyeti feki  (vyeti vya kughushi) na watumishi wanaotumia cheti kimoja kwa watumishi wawili na zaidi. Taarifa ya serikali ilisema watumishi takribani 9,000 wamegundulika kutumia vyeti vya kughushi, wakati watumishi takribani 1,000 wanatumia cheti kimoja watu wawili au zaidi. Sambamba na hilo la watumishi wenye mapungufu, Serikali ilitoa majina kwa kila mkoa ya watumishi waliohakikiwa na kuonekana wana vyeti halali kuanzia sekondari hadi vyuoni. Zoezi hili lilitumia muda na pesa nyingi za watumishi, pamoja na pesa za umma. Kipindi chote cha uhakiki, haki za watumishi wa umma hususani maslahi ya mshahara, madeni, nyongeza ya mwaka (salary increment), upandishaji wa madaraja nk. vyote vilisimama hadi sasa mwaka wa pili umetimia. Kwa mantiki hiyo hawa watumishi kwa ujumla nchini ambao wameonekana kuwa na vyeti halali baada ya uhakiki wa muda mrefu kufanyika na kukam

MEYA WA MANISPAA YA UBUNGO MH BONIFACE JACOB AZINDUA KITUO CHA KIPYA CHA KIELETRONIKI CHA KULIPA

Image
Mstahiki Meya Jacob Boniface akiwa katika uzinduzi Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ubungo, Boniface Jacob, leo Ijumaa 30 Julai 2017, amezindua kituo cha kisasa cha kukusanya kodi, ushuru na tozo mbalimbali katika eneo la Simu 2000. Hii itapunguza kero kwa  wananchi wanaoishi maeneo ya karibu na eneo la Simu 2000, kulipa kodi, ushuru na tozo mbalimbali ambapo awali walilazimika kwenda Kibamba zilizopo ofisi za Manispaa ya Halmashauri ya Ubungo. Kituo hiki kipya kinategemea kuwasaidia wakazi wa Sinza, Mabibo,  Makuburi, Ubungo na maeneo yote ya karibu.

BREAKING NEWS: MH EDWARD LOWASSA ATAKUWEPO MAKAO MAKUU YA JESHI LA POLISI LEO SAA SITA MCHANA

Image
Waziri Mkuu wa zamani Mh Edward Lowassa leo akuwepo Makao Makuu ya Jeshi la Polisi kujua hatma ya tuhuma zinazomkabili juu ya uchochezi .Mh Edward Lowassa anatarajia kufika makao makuu ya Jeshi la Polisi mnamo majira ya saa 6 mchana kama alivyoelekezwa na Jeshi hilo hilo la Polisi.,Inasemekana atasindikizwa na Polisi kutoka nyumbani kwake hadi makao makuy ya jeshi la polisi. Endelea kufuatilia kwa karb upate habari zaidi

SULEIMAN MATHEW ALIMAARUFU MESI NA MWENZAKE WAPETA KATIKA HUKUMU YA RUFAA

Image
Na Nkatunga Philibert Mahakama Kuu Kanda ya Mtwara imewaachia huru Suleiman Mathew (Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Lindi) na mwenzake Ismail Kupilila (Katibu wa CHADEMA Tawi la Nyangamara). Viongozi hawa walikuwa wamehukumiwa adhabu ya kifungo miezi nane jela bila faini na Mahakama ya Wilaya ya Lindi mnamo 18.01.2017. Baadae walikata rufaa Mahakama Kuu na kuomba dhamana kwa hati ya dharua ambayo walipewa tarehe 07.03.2017. Wakati anasoma hukumu hiyo Jaji Mlacha alisema kwamba kosa la kusanyiko lisilo halali linatakiwa kufanywa na watu watatu au zaidi sio wawili. Akasema pia kwamba vifungo vyao vimefutwa. Wako huru kwa sababu hawana hatia. Aliongeza kusema kwamba ameona mambo kadha katika kesi hii (Observations) 1. Kwa mujibu wa sheria Jeshi la Polisi halina mamlaka ya kutoa vibali kwa vyama vya siasa kuhusu mikutano au maandamano kama ambavyo aliyekuwa OCD Ngiichi alidai katika ushahidi wake. 2. Warufani wameelekezwa kutoa taarifa Polisi kama sheria inavyotaka na si kwa Mtendaji

Ulipaji wa madeni ya watumishi wa umma, ufanyike kwa kasi kama uhakiki wa vyeti ulivyofanyika!

NA RUSTON MSANGI. Tangu serikali ya awamu ya tano iingie madarakani mwezi octoba 2015, takribani miaka 2 hadi sasa kumekuwa na misamiati maarufu kama UHAKIKI na UTUMBUAJI majipu. Hivi vyote vikienda sambamba kwa lengo la kuhakikisha watumishi wa umma waliopo makazini wana vigezo vyote ikiwemo kigezo kikuu cha kitaaluma. Lengo lake ni zuri japo ya mapungufu na usumbufu mkubwa uliojitoekeza kwa watumishi wa umma hasa wale waliokidhi vigezo vyote. Uhakiki umepelekea wengi kufukuzwa, kuacha kazi lakini na wengine kubaki kwenye nafasi zao. Uhakiki kwa watumishi wa umma ikiwemo walimu ambao ndio watumishi pekee wengi nchini kuliko kada yoyote ile, umesababisha usumbufu mkubwa sana hasa wa kiuchumi na haki nyingi za msingi za kisheria kusimamishwa, wakati watumishi wakiendelea kutimiza wajibu wao wa kazi katika majukumu ya kila siku. Mfano walimu wastaafu na waliostahili kupanda madaraja pekee wanaidai serikali zaidi ya bilioni 300. Mbali na usumbufu huu kwa watumishi wa umma n

Watumishi wa umma nchini Tanzania wanaongoza kutokuwa na furaha!

Pigo jingine kwa walimu na watumishi wa umma kwa ujumla

Image
NA RUSTON MSANGI. Katika watumishi wa umma, ualimu ni kada pekee yenye watumishi wengi kuliko kada yoyote ile nchini. Ni kada mojawapo yenye changamoto nyingi pengine kuliko kada yoyote ile. Tangu utawala wa awamu ya 5 uingie madarakani chini ya Rais Magufuli, matatizo ya watumishi wa Umma hususani walimu yamekuwa maradufu ya mwanzo. Mtakumbuka kwamba tangu kuanza kwa zoezi la uhakiki usioisha, haki nyingi za walimu zimesimamishwa bila kufanyiwa kazi huku kukiwa na manyanyaso, ukandamizwaji na uonevu usio na mwisho kupitia kwa watendaji mbalimbali serikali kuu, halmshauri na baadhi ya maeneo kutoka kwa serikali za kata na vijiji. Madaraja ya mishahara yamesimama, uhamisho umesimama, ongezeko la mshahara (salary increment ) kwa mujibu wa mkataba wa kazi umesimama, madeni hayalipwi, makato yameongezeka maradufu. Mbali na yote hayo, walimu wameendelea kutimiza wajibu wao na hata kulaumiwa kwa matokeo mabovu ya shule za serikali. Kabla ya hata kupanda kwa  makato ya 15%

Walimu wa mwaka 1993 ni mfano wa kuigwa

NA RUSTON MSANGI. Katika historia ya harakati za walimu nchini, inaonesha kwamba mwaka 1993 kulitokea mgomo wa walimu. Kipindi hiki ulikuwa utawala wa awamu ya pili chini ya Rais Ally Hassan Mwinyi. Mgomo huu ulitokana na madai lukuki ya walimu dhidi ya Serikali, kama ilivyo sasa. Kinara wa mgomo huo alikuwa Mwalimu Peter Lebabu Mashanga, huyu alikuwa ni mwenyekiti wa OTTU (Organization of Tanzania Trade Unions) tawi la Azania sekondari. Mwalimu Peter Lebabu Mashanga akiungwa mkono na walimu wa Dar es Salaam mnamo October 1993, walimuandikia Rais Ally Hassan Mwinyi barua, wakieleza madai 14 ya walimu na kumpa muda maalum wa kutekeleza madai hayo. Vinginevyo wangegoma nchi nzima ikifika 1/11/1993 hadi madai yatakapotekelezwa. Madai haya ya walimu ya mwaka 1993 yalijulikana kama ''Pan African Tanzania Teachers Demands''. Na madai yenyewe baadhi ni kama ifuatavyo:- 1. Comprehensive medical care. 2. Emergency medical fund amounting to 60,000 p.m 3. Lunch

Vyama vya wafanyakazi vijifunze kwa Kituo cha Sheria na Haki za binadamu LHRC!

NA RUSTON MSANGI. Ni jukumu la kila chama cha wafanyakazi nchini  kusimamia, kulinda, kuboresha maslahi, na kuhakikisha haki za wanachama wake hazivunjwi, wala kukiukwa kwa namna yoyote ile. Majukumu hayo ya chama chochote cha wafanyakazi hayaepukiki kwa kuwa wanachama huwa na utaratibu maalumu wa kuchangia kwa njia ya ada, ili kufanikisha shughuli za chama husika. Mfano wa vyama vya wafanyakazi nchini ni kama Chama cha walimu Tanzania (CWT), Muungano wa wafanyakazi katika sekta ya viwanda na biashara (TUICO), Umoja wa wafanyakazi wa afya wa serikali (TUGHE), Muungano wa wafanyakazi wa Serikali za mitaa (TALGWU). Mwezi huu umekuwa ni pigo kwa wafanyakazi nchini, hasa wale walionufaika na mikopo ya elimu juu wakati wa masomo yao. Maumivu haya makubwa ni kuhusu mabadiliko ya sheria yaliyopelekea kuongezeka kwa makato ya marejesho ya mikopo, kutoka 8% ya awali hadi 15% iliyoanza kukatwa mwezi huu wa pili. Suala hili kiukweli limewaacha wafanyakazi wengi nchini na maumivu mak

Elimu bure imekuza tatizo la chakula mashuleni

NA RUSTON MSANGI. Ubongo wa mwanadamu ili ufanye kazi sawa sawa na kwa ufanisi,unahitaji lishe.Ni muhimu kula vizuri na kushiba. Mwanafunzi darasani,anatumia  akili nyingi.Ili aweze kufikiri vizuri na kuelewa anachofundishwa ni lazima apate chakula kwa muda sahihi na kushiba.Ni muhimu. Kabla ya waraka wa elimu bure wa serikali ya awamu na tano  mwaka 2016, wanafunzi katika shule nyingi za serikali walikuwa wanakula shuleni kutokana na michango ya  wao. Baada ya waraka wa elimu bure kuanza kutekelezwa rasmi mwaka jana 2016,kumetokea  mabadiliko makubwa ya hali ulaji wa chakula mashuleni.Wanafunzi hawali kama mwanzo. Waraka wa elimu bure umeainisha  majukumu ya serikali,  wizara ya elimu, TAMISEMI, Halmashauri, Wakuu wa shule na walimu Aidha umeanisha majukumu ya mzazi katika kutekeleza elimu bure. Mojawapo ya majukumu ya wazazi ni kuhakikisha mtoto/mwanafunzi anapata vifaa vyote muhimu vya shule kama madaftari na sare za shule . jukumu jingine kubwa na muhimu kwa wa