Posts

Showing posts from June, 2015

UKAWA INATAKA KUSHINDA AU KUSHIRIKI UCHAGUZI MKUU MWAKA HUU 2015?

Image
UKAWA inataka kushinda Uchaguzi au inataka Kushiriki Uchaguzi? Yericko Nyerere  Kushindwa kwa upinzani nchni kwa kiwango kikubwa katika chaguzi hizi kunatokana na muundo wa vyombo vya maamuzi ya uchaguzi wa nchi yetu, mathalani, Katiba, Tume. Kwasasa Katiba inasema kuwa matokeo ya urais hayatahojiwa na mtu yeyote ama chombo chochote wala mahali popote, hii inamaana kuwa Mwenyekiti wa Tume anayechaguliwa na Mwenyekiti wa CCM na anayelipwa na Mwenyekiti wa ccm akitangaza jina fulani hata kwa bahati mbaya tu baai haruhusiwi kurekebisha. Mwaka 2010 baada ya kushindwa uchaguzi mkuu, Upinzani chini ya Chadema uliituhumu sana tume Uchaguzi kwakuchakachua matokeo ambayo ilipoka ushindi wa 64% wa Dr Slaa malalamiko yao ndiyo yalipelekea kuwepo mchakato wa kuandika katiba mpya. Mchakato huo umeishia kwa zengwe la CCM kuvuruga maoni ya umma na kuweka maoni yao ambayo ni kinyume kabisa na matakwa ya umma, Maridhiano ya upinzani na msanii wa ccm baada ya dalili za uwepo finyu wa kati

Mh.KAFULILA AWALIPUA MAWAZIRI UFISADI MABEHEWA, ALITAKA BUNGE KUWAJIBISHA VIGOGO UFISADI WA MABEHEWA

Image
Na Shindo Kilawa Pichani ni Mh KAFULILA 

BENSON KIGAILA AONESHA UWEZO WA KIPEKEE KATIKA KUPAMBANUA MAMBO

Na Mhere Mwita Majira ya saa 2:30 Ndugu Benson Kigaila ambaye ni mkurugenzi wa organization ya CHADEMA ngazi ya Taifa na ni mtia nia ubunge jimbo la Dodoma mjini alifanikiwa kufanya mdahalo na wanachama ,baadhi ya viongozi na watia nia wa  Ubunge na Udiwani toka sehemu mbalimbali za nchi.Kijana haya alijidhihirisha kuwa anauwezo wa kipekee na ana kaliba ya kiuongozi kwa kujib maswali kwa ufasaha zaidi ya matarajio ya wengi. Uwezo wake ulitambulisha kuwa CHADEMA ina hazina kubwa ya viongozi tens waliomakini nitaweka baadhi ya maswali na majibu aliyoulizwa na wajumbe hao hapa chini:- swali 1:Kwanini umeamua kugombea ubunge? Majibu:Nimeamua kugombea ubunge kwa lengo la kusaidia kujenga jamii ya watu walio sawa mbele ya sharia,jamii guru na inayongozwa kwa haki na kuwatatulia kero zinazowakabili sasa ambazo waliopita hawajazitatua hadi leo kwa mfano Tatizo la Ardhi ya watu wa Dodoma dhidi ya CDA,ni tatizo kubwa linalohitaji mtu anayelijua na ana dhamira ya dhati kulitatua aliweka u

RAIS WA MAREKANI BARAKI OBAMA AKERWA NA MAUAJI YA WAMAREKANI WEUSI, AMESIKITISHWA SANA NA KITENDO HICHO CHA KIKATILI NA KIBAGUZI

Image
Rais wa Marekani (USA) Barak Obama amesema mauaji ya watu tisa ndani ya Kanisa Wamarekani Weusi katika eneo la Charleston, jimbo la Carolina Kusini yanaibua maswali mengi sana Aidha Mh Barak Obama amesema chuki miongoni mwa jamii kwa misingi ya rangi na imani ni kitisho kwa demokrasia ya Marekani amelaani vikali kitendo hicho na vitendo vingine vinavyoweza kuhatarisha umoja wao, ameyasema hayo mda mfupi baada ya kijana wa kizungu aliyehusika kufanya mauaji hayo ya watu tisa kukamatwa. Pia ametaka kufanyika kwa mabadiliko ya pamoja katika fikra za Wamarekani kuhusu ghasia zinazosababishwa na matumizi ya silaha.

KAFULILA: JK KAVUNJA MISINGI YA UCHUMI ALOWEKA MKAPA.

Image
Na Mh Kafulila Huu ndio mchango wangu bungeni jioni leo.Mkapa aliweka misingi ya uchumi mkuu( macro economics) kilichopaswa kufanywa na JK ni kuhakikisha mafanikio hayo yanajitokeza kwenye uchumi wa kawaida ili kila mtanzania aone fahari ya kukua kwa uchumi wake lakn bahati mbaya amebomoa kabisa na sasa inabidi UKAWA tuanze upya baada ya uchaguzi Oct. 1. Mkapa amepokea nchi mwaka 1995  ukuaji wa uchumi ukiwa 4.2 akakuza mpaka 6.7 mwaka 2004. Leo JK kashusha uchumi mpaka 6.4 mwaka 2014. 2. Amepokea nchi riba ya mabenki ikiwa 30-26% mwaka 1995 lakn mwaka 2005 riba za mabenki ilishuka hadi 14% lakn leo JK riba zimepanda mpaka 18%. Hii inathiri sana ukuaji wa sekta binafsi na biashara nchini. 3.Mwaka 1995 mfumko wa bei ulikuwa 21% lakn mwaka 2005 mfumko ulishuka mpaka 4%. Leo JK mfumko wa bei ni 5.3% .  4. Mkapa kapewa nchi mwaka 1995 akiba ya fedha za kigeni zikiwa za miezi 2 lakn mwaka 2005 akiba ilikuwa ya miezi 8 lakn leo mwaka 2015 akiba za pesa za kigeni zinato

HEKAHEKA ZA WANAVYUO NA NEC KUHUSU KUJIANDIKISHA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA

Image
Na Alex Elifurah Kweli vyuo vikuu tukinyamaza na kutokupiga kura October 2015,itabidi tupimwe akili au tupewe chanjo ya Akili, Kuelekea October  hii chanjo ni muhimu sana. waraka wa vyuo vikuu kuomba hatma yao kuelekea uchaguzi mkuu umewasili kwa Jaji Lubuva,Mwenyekiti wa Tume ya taifa ya uchaguzi, na tumefanya NAE mazungumzo ya pamoja na ametupa mrejesho kwa maandishi. Lazima  vyuo vikuu vijiandae kisaikolojia kupoteza haki yao ya msingi ya kupiga kura kwani majibu ya waraka ule una mapungufu mengi sana. Mahojiano kati yetu na mwenyekiti wa  Tume ya uchaguzi kwa kupitia vyombo mbalimbali vya habari moja kwa moja amedai zoezi limefeli hivyo ni mapungufu yao. Maamuzi yetu ni kufungua shauri mahakamani na kupeleka waraka kwa tume ya haki za binadamu baadaya ya Tar 18. August 2015 ambayo ni mwisho ya kuboresha na kuhamisha Taarifa kwa wapiga kura. Pia kutokana na  rekodi za utendaji mbovu wa tume kwanzia kura za maoni ya katiba,uandikishaji na ukusanyaji wa  taarifa k

Mh. KAFULILA AFUNGUKA KUHUSU ZITTO& ESCROW

Image
Na Shindo Kilawa Pichani ni Mh David Kafulila Mbunge (NCCR MAGEUZI)  wa kiwa na mke wake Kamanda Jesca Kishoa Kutoka Singida baada ya kupokea zawadi.  Leo asubuhi katika kundi la watsap la IPTL BRING BACK OUR MONEY(IBBOM) liloundwa kipindi cha sakata la Escrow na vijana wapambanaji. Mh Kafulila alipohojiwa na vijana hao ndani ya kundi hilo juu ya Zitto Zuberi Kabwe kama alimsaidia katika kampeni za mwaka 2010 jimboni kwake, kama wanavyosema wapambe wa ZZK. Mh Kafulila akaamua kufunguka, namnukuu "Naomba kuweka kumbukumbu sawa tu kwamba Zitto ni rafiki yangu tangu nikiwa chadema lakini haimanishi tunakubaliana kila kitu. Naudhika kuona wafuasi wake wakiandika uongo ambao hata yeye mwenyewe zitto anajua ni uongo kwamba alinisaidia kwenye kampeni" Akaendelea kwa kusema "Ukweli wa Mungu zitto hakunisaidia hata lita ya mafuta kwenye kampeni kwasababu anazojua yeye ambazo nisingependa kumsemea. Aliahidi tu kwenye magazeti. Labda wafuasi wake wamrudie kumuuliza vizur

PERUZI MAGAZETI YA LEO Tr 18/06/2015

Image

CCM WANAPENDA NAMBA LAKINI HAWAJUI HESABU.!

Image
Na Malisa GJ, Leo tuongee uchumi kidogo. Kuna watu wanapenda namba lakini hawajui hesabu. Kama na wewe ni mmoja wao tafadhali usisome makala hii. Wabunge wengi na mawaziri wa chama cha mapinduzi ni wagonjwa wa namba. Wanapenda namba lakini hawajui hesabu. Ukitaka wakushangilie we ongeza tarakimu tu kwenye namba. Wanapenda namba lakini hawajui hesabu.! Kama ulikua unamlipa mtumishi mshahara wa laki 5 mwaka jana mwaka huu mlipe laki 7. Atashangilia na kukushukuru. Kumbe hajui upande wa pili gharama za maisha zimeifanya hiyo laki 7 iwe sawa na laki moja ya mwaka jana. Yeye atakushukuru tu, kwa sababu anapenda namba lakini hajui hesabu.! Naona wengi hamjanielewa. Ni hivi kuna faida gani kulipwa mshahara wa milioni mbili halafu ukauziwa sukari kilo moja sh.3000/=??? Si bora ulipwe laki 5 sukari uuziwe sh.500/= kwa kilo. Kama unapenda namba lakini hujui hesabu huwezi kunielewa. Twende kwenye historia kidogo. Mwaka 2005 wakati Rais Mkapa anaondoka madarakani bajeti ya serikali

PERUZI MAGAZETI HAPA KILA SIKU

Image

HATIMAYE JIMBO LA RUNGWE MASHARIKI LAPATA MKOMBOZI WAO ATAKAYEWATETEA.

Image
Dr Elias akiwa katika mkutano na wananchi  wa kata ya Isange.  Pichani ni Dr Elias akiwahutubia wananchi wa kata ya Isange.  Dr Elias akiwa na wananchi wa kata ya Lutabe jimboni kwake Rungwe mashariki, nyumba kwa nyumba, shamba kwa shamba operation aliyoifanya kwa mienzi zaidi ya miwili hadi sasa anaendelea na operation hii ili kuwakombowa wakazi wa RUNGWE Hakika penye nia pana njia,jimbo la Rungwe mashariki liliongozwa kwa mda mrefu na mh Prof. Mark Mwandosya lakini hakuweza kuwasemea wananchi matatizo yao bungeni kwa mda mrefu, sijui kwakuwa alikuwa ni Waziri japo sio sababu ya kushindwa kuwasemea wananchi wa jimbo lake. Inasemekana Mh Mwandosya  kashindwa kabisa kuwatetea wakulima wa chai huku akijua kabisa chai ni zao muhimu la biashara kwa wakazi wa Rungwe, lakini hadi sasa wanauza kwa bei ya hasara sana kwa kilo. Lakini pia kama  mbunge hajafanya jitihada za kufufua na kuboresha kiwanda cha chai kilichoko Mwakaleli, hivyo kuwanyima fursa za ajira wakazi wa Bus

OMBWE LA AJALI ZA BARABARANI LAIBUKA TENA MKOANI IRINGA

Image
Ni muonekano wa gari ubavuni baada ya kupata ajali eneo hilo la kinyanambo, Mafinga Kama unavyoona katika picha hizi, hivi ndivyo gari lilivyosambaratishwa baada ya ajali iliyoleta maumivu makali na kuacha majuzi kwa taifa letu. Pichani ni Muonekano wa Gari aina ya Coaster la Another G baada ya kupata ajali eneo hilo la Kinyanambo, nje kidogo ya mji wa Mafinga wilayani Mfindi Katika ajali iliyotokea usiku wa jana japo eneo la Kinyanambo,Mafinga wilayani Mfindi katika barabara kuu nje kidogo ya Mji wa Mafinga.  Imeripotiwa Kuwa watu 23 wamepoteza maisha na wengine 34 kujeruhiwa vibaya. Mashuhuda wa ajali hiyo wamesema gari aina  ya costa mali ya Another G inayofanya  safari  zake kati ya mikoa ya Iringa na Njombe ilikuwa ikitokea Iringa mjini kuelekea Njombe iligongana na lori la mizigo na kusababisha maafa hayo. Aidha Mkuu  wa wilaya ya  Mufindi Miss.  Mboni Mhita amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo  na  kueleza kuwa hii ni miongoni mwa ajali  mbaya ku

SHEIKH MKUU MUFTI ISSA BIN SHAABAN SIMBA AFARIKI DUNIA

Image
Mufti, Shekh mkuu  Tanzania Issa Bin Shaabani Simba enzi za Uhai wake.  Taarifa zilizotufikia hivi punde ni kwamba Sheikh Mkuu wa Tanzania Mufti Issa Bin Shaaban Simba amefariki asubuhi ya kuamkia leo majira ya saa nne kasorobo., Inasemekana kaaga dunia katika hospitali ya TMJ jijini Dar es salaamu alikokuwa akipatiwa matibabu. Huu ni msiba mkubwa kwa watanzania wote kwani alikuwa ni nguzo kubwa katika kudumisha amani ya nchi yetu. Mwenyenzi Mungu ailaze mahala pema roho ya Marehemu Sheikh Mkuu, Mufti Issa Bin Shaabani Simba. Na awape nguvu waislamu wote nchini Tanzania na ulimwengu mzima kwa kufikwa na msiba huu wa kuondokewa na kiongozi wao mkuu. R. I. P

UKISTAAJABU YA WANAWAKE WA ROMBO UTAYAONA YA WIZARA YA UCHUKUZI NA STESHENI YA RELI MOSHI MJINI.

Image
Na Mwl. Denis Bongole Hili ni Daraja la Tsavo nchini kenya, ujenzi wa mradi huu unaendelea hadi sasa Hapa ni Stesheni ya Gari moshi iliyopo mkoani Kilimanjaro, Moshi Wiki chache zilizopita gazeti la mwananchi linalomilikiwa na kampuni ya Mwananchi communication limited lilimnukuu mkuu wa wilaya ya rombo akisema kua eti "wanawake wa rombo wanakodi wanaume wakenya kutoa huduma za kindoa" Binafsi sikuona ajabu sana ila nilitafsiri kama 'vita ya kisiasa' dhidi ya mbunge aliepo sasa ndugu Joseph Selasini. Nilipata kuandika hapa juu ya hili hivyo leo nataka tuunganishe matukio katika sakata la aina yake ndani ya wizara ya uchukuzi. Majuzi hapa Raisi wa Kenya bwana Uhuru Kenyata aliandika katika ukurasa wake wa facebook kuhusu safari yake na mawaziri kadhaa ambapo walionekana katika picha wakiwa wametembelea "daraja la tsavo" kukagua ujenzi wa reli ya kisasa kabisa nchini humo. Cha ajabu zaidi ni mwaka mmoja tu toka achaguliwe ambapo pamoja na misu

RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO TANZANIA MH. PROF. DR. JAKAYA MRISHO KIKWETE AMEWASILI JOHANNESBURG NCHIN AFRIKA KUSINI KWA AJILI YA MKUTANO WA UMOJA WA AFRIKA

Image
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa ameongozana na mkewe mama Salma Kikwete(hayupo pichani) wakilakiwa na maofisa wa Ubalozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini mara walipowasili katika hoteli ya Sun Internatioal Maslow Hotel, Sandton, Johannesburg, Afrika ya Kusini kwa ajili ya kuhudhuria Mkutano wa 25 wa kawaida wa Umoja wa Afrika. PICHA NA IKULU PICHA ZOTE KWAHISANI YA IKULU

ALLY KIBA AMBWAGA DANGOTE

Image
Tuzo za Kilimanjaro Tanzania Music Awards (KTMA) zimemalizika huku Ally kiba akionekana mwiba mkali baada yakufanikiwa kuchukuwa tuzo tano binafsi na nyingine wakichukuwa pamoja na Mwana FA katika kipengele cha wimbo bora wakushirikishwa.Watu wengi walimtabiria ushindi mnono Diamond lakini mambo yakawa sivyo ndivyo na Kiba kuibuka Kidedea Katika tuzo hizo ushindani mkubwa ulitarajiwa kuibuka baina ya Nassib abdul na Ally kiba ila hali ilikuwa tofauti kwani Kiba alijikuta akibeba tunzo hizo tano na wimbo wake wa mwana Dar es salaam katika vipengele ivyo vitano ikiwepo cha wimbo bora wa Afro Pop, mtunzi bora wa mwaka, na wimbo bora wa mwaka, hali iliyopelekea mashabiki wa Diamond kulalamika kuwa kuna upendeleo uliofanyika, Mashabiki hao wameonekana wakilalamika katika mitandao mbalimbali ya kijamii huku mashabiki wa Alikiba wakitamba na kufurahia ushindi. Aidha mshindani wa karibu wa Kiba, Diamond amepata tunzo mbili tu katika eneo la wimbo bora wa zuku na rumba kupitia wimbo wa &

MH HALIMA MDEE AIBUKA KIDEDEA DHIDI YA SERIKALI JUU YA MGOGORO WA ARDHI JIMBONI KWAKE KAWE ENEO LA CHASIMBA

Image
Na Shindo Isaac Aliyesimama ni Mh Halima Mdee Mbunge wa Kawe kupitia CHADEMA,  kulia kwake ni Waziri na naibu wake  Wananchi wakisikiliza mwafaka wa mgogoro wa ardhi katika makazi yao, hakika wameona ukombozi kupitia chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA.  Mh Halima Mdee akiongea na makamanda wake, kushoto kwa Mh Halima Mdee ni mwanadada chipukizi katika siasa Eng. Pamela Maasay, Mwenyekiti BAVICHA jimbo la kawe,  Vijana hawa kwa ujumla wameiva haswaaa kuutafuta ukombozi Hatimaye leo Mh Halima Mdee ametangaza rasmi ushindi dhidi ya serikali dhalimu ya chama cha mapinduzi (CCM) juu ya mgogoro wa ardhi uliodumu kwa mda mrefu katika kata ya Bunju Chasimba, serikali imeamua kunyoosha mikono na kuwaachia wananchi hao kuendelea na maisha yao kama ilivyokuwa kabla ya mgogoro. Hakika mwanadada huyu ambaye ni mbunge wa Kawe na mwenyekiti BAWACHA taifa kaonesha na kadhihirisha kuwa ana uwezo mkubwa na anafaa kuendelea kuwatumikia wana wa Kawe. Kashirikiana vyema na madiwan

MAALIMU SEIF AAHIDI KUNGANISHA UNGUJA NA PEMBA ENDAPO ATACHAGULIWA

Image
Makamu wa kwanza warais wa Zanzibar na mgombea wanafasi ya urais kupitia chama cha wananchi CUF Maalimu Seif Sharifu Hamadi ameahidi kuwaunganisha wakaz wa visiwa vya unguja na pemba. Ahadi iyo ameitoa mchana leo katika viwanja vya Timiliza, Chakechake Pemba wakati wakutambulishwa kama mgombea wakiti cha Urais kupitia tiketi ya chama cha CUF Zanzanibar. Maalim Seif amesema endapo wanachi watampa ridhaa yakuwa Rais atahakikisha anaweka boti ambazo zitafanya safari zake kati ya Unguja na Pemba wakati wote ili wakulima waweze fanyabiashara zao kwa urahisi zaidi. Amesema kuwa uwepo wa boti izo itasidia shughuli mbalimbali katika jamii ya watu wa zanzibari nakusema kuwa ndio njia pekee itakayoleta mwilingilino baina ya waunguja na wapemba. Aidha Maalim Seif amesema kwasasa wazanzibari wanatakiwa kuwa wamoja ili waweze kukiondoa Chama Cha Mapinduzi(CCM) ambacho kimeonekana kushindwa kuleta umoja. "Nduguzangu sasa nikipindi chakuwa pamoja na kuhakikisha tunaungana ili tuweze k

MICHEZO

Image
NJE NDANI KATIKA SOKA No.1. ...Timu ya chelsea ni iliyofanikiwa kuwa bingwa wa wingereza kwa msimu huu ulioshia,pamoja na yote tmu hii ilitoka kwenye ukata mkubwa wa kikombe cha uingereza kwa takribani miaka mitano iliyopita.kuna jambo moja lilikuwa linatokea kwa bosi mkubwa kutokuwa na mahusiano mazuri na mameneja wake kwa kuingilia utendaji wa kazi zao...hakika nadiriki kusema hakuna kocha wa chelsea alifukuzwa ambapo alistahil kufukuzwa zaidi ya andreas villa boas,baada ya majuto yote hayo abromovichi aliamua kumfuata morinyo na kupewa masharti ya kutoingiliwa kwenye timu.baada ya miaka miwili mmorinyo kukabidhiwa timu amechukua ubingwa wa baclays huku akipewa ushirikiano wa hali ha juu na boss wake pamoja na kurugenzi nzima ndani ya tmu.alitulia akasajili pale palipostahili kuziba nafas timu ikawa na nguvu kubwa. 2.Tunawachezaji wengi timu ya taifa lakini wote ukiwauliza ndoto zao watakwambia nataka kucheza simba na yanga na nifanye vizuri timu ya taifa,ni aibu kwa kwe

DAR-ES-SALAAM STAND UP..... NI BAVICHA DADAZ M4C COMMANDOZ OPERATION, MOSHOST MPOOOO, UNGANA NASI KWA UKOMBOZI THABITI

Image
DAR-ES-SALAAM STAND UP .....! MASHOSTI MPOOOO....???? Mwanamke akiwasaidia wananchi kijitambua na kuyakubali mabadiriko katibu wa BAVICHA jimbo la Kigambon kamanda Nusrat Hanje na team ya wadada machachari kutoka mkoa wa DAR-ES-SALAAM wanawaletea operation maalum kwa ajil ya mkoa wa DAR-ES-SALAAM na viunga vyake vyote kwa ajil ya kuhamasisha wasichana wengi kujiandikisha kwenye daftar la kudumu la wapiga kura BVR. Operation itaitwa DAR-ES-SALAAM BAVICHA DADAZ M4C commandoz... Kauli mbiu ni "Shosti JIANDIKISHE" Operation hii maalum itafanyika jiji Zima kwa mpangilio wa majimbo nane naitaanzia jimbo la Kigambon siku ya jumatano tar. 10/06 /2015 nakuendelea majimbo mengine kwa siku Tano mfululizo. Operation itahusisha kufanya mkutano midogo midogo maeneo yenye mikusanyiko ya watu wengi nawahutubiaji ni wadada wenyewe. ili kufanikisha zoez hili unaweza kuwachangia wasichana Hawa wa Chadema mafuta kupitia kiongoz wa operation kamanda Nusrat Hanje. MUNGU awabar

UTAMTENGANISHA VIPI MAKONGORO NA WANACHAMA PAMOJA NA VIONGOZI WENGINE NDANI YA CCM?

Image
Unamtenganisha vipi Makongoro na wanachama pamoja na viongozi wengine ndani ya CCM?  Na Yericko Nyerere Ni baada ya Msafara wa Makongoro kuelekea Kigoma kupata ajali Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inamka kwamba, Tanzania ni nchi ya mfumo wa vyama vingi, rais atachaguliwa kutoka kwenye chama cha siasa, hii inamaana kuwa ni lazima awe mwanachama wa chama cha siasa.  Katiba ya chama cha mapinduzi inasema kuwa ili uwe mwanachama, ni lazima ukubaliane na Itikadi,falsafa na miiko ya chama cha mapinduzi. Sasa ili chama kiongoze serikali hutumia sera, sera ndio dira ya kuongozea serikali ya chama.  Ili chama kunadi sera zake huwa kinatanguliwa na Ilani, ilani ya chama ndio dira ya kunadia sera za chama husika mbele ya makutano. Hilo ndilo lilipo kwa vyama vyote vya kidemokrasia duniani.  Ndani ya ccm mwaka huu wa uchaguzi Ilani na sera yake inaandaliwa na makada mashuhuri wa chama hicho wakiongozwa na Andrew Chenge, Steven Wasira, Asha Rose Migiro, na wajumbe wengine

BUNGE LIMEKULA MATAPISHI YA ESCROW

BUNGE LIMEKULA MATAPISHI YA ESCROW Leo kwa mara ya kwanza wabunge wa ccm wameshangilia waziri wa nishati kukanyaga maazimio ya Bunge kuhusu ESCROW. Iliibuka baada ya mwasisi wa hoja mhe Kafulila  iliyompatia tuzo kwa kusimama bila kuyumba Mhe kafululila alihoji kwann serikali iendelee kumlipa singasinga tozo ya uwekezaji dola 2.6m( bilioni5) kama gharama ya uwekezaji kila mweza sawa na 60bn kwa mwaka kwa muda usiojulikana. Kafulila alihoji uhalali wa malipo hayo ilhali azimio la bunge ni mitambo hiyo kutaifishwa na zaidi ripoti ya cag ilibainisha wazi kuwa singasinga huyo manunuzi aliyafanya kwa nyaraka za kugushi ambayo ni jinai achilia mbali wizi wa pesa. Simbachawene alijibu kuwa serikali haiwezi kutekeleza azimio hilo la bunge kwa hoja kuwa serikali itashtakiwa. Na wabunge wa ccm kumshangilia huku wakimzomea kafulila utadhani hayakuwa mazimio ya bunge. Kafulila alisimama na kusisitiza kuwa kiti cha spika kuanzia makinda na hata zungu wamekuwa wakimdhibiti kuhakikisha ha

KAMANDA JESKA KISHOA AKAMATWA NA POLISI KWA SHINIKIZO LA MBUNGE WA IRAMBA MASHARIKI MH MWIGULU NCHEMBA, NI AIBU YA MWAKA KWA MKUU WA WILAYA NA NAIBU WAZIRI WA FEDHA

Image
Ni aibu ya mwaka kwa nchi inayojinasibu kuwa ya democrasia huku mawaziri wake wanatumia vibaya dhamana zao. Pichani ni Kamanda Jesca Kishoa akiwaambia jambo polisi Kamanda Jesca Kishoa akiwa na makamanda wengine  Ni ushauri wa bure kwa mawaziri wa serikali yetu inayotawala kwa sasa waache tabia za kutumia dhamana walizopewa kuminya na kukandamiza demkrasia ya nchi kwa hofu za kuondolewa madarakani. Walipaswa kufanya kazi zinazowanufaisha wananchi na wao wangeamua kama wanafaa au la? Aibu hii imekuwa ikijitokeza sehemu nyingi za nchi yetu hasa majimbo waliyotoka mawaziri au manaibu waziri wa serikali ya ccm. Lakini je ni kwanini wajihami kwa kutumia polisi? Na ni kwanini polisi nao wakubali kutumika? Kwanini wasifuate maadili ya kazi zao. Nasema ni aibu kwa sababu kubwa moja iliyonifanya kuandika hapa kila mmoja ajue siku ya lea kamanda wa chadema Jesca kishoa ambaye ni Mke wa Mh. David kafulila (mbunge) amekamatwa na polisi kwa shinikizo la Mwigulu Nchemba  ifahamike ku