Posts

Showing posts from August, 2016

KUCHELEWA KWA AJIRA KUNAVYOUMIZA WALIMU

NA RUSTON MSANGI. Kada ya ualimu ndiyo yenye watumishi wengi nchini kuliko kada yoyote ile. Licha ya kada hii kuwa na watumishi wengi,takwimu zinaonesha bado kuna upungufu wa walimu nchini hasa walimu wa sayansi . Waziri mwenye dhamana ya  elimu,Profesa Joyce Ndalichako akijibu swali katika kikao cha bunge kilichopita, alibainisha upungufu wa walimu wa Sayansi 22,460. Miaka kadhaa iliyopita,watu wengi wamepata hamasa ya kusomea fani ya ualimu ili waajiriwe na serikali.Hakika walimu wamekuwa wakiajiriwa moja kwa moja katika shule katika shule za msingi na sekondari na vyuo . Walimu wamekuwa wakiajiriwa kwa vipindi tofauti mara wa wanapohitimu. Kwa mfano, walimu waliohitimu mwaka 2012 walipangiwa vituo vya kazi mwezi Februari 2013. Waliohitimu mwaka 2013 walipangiwa mwezi Machi 2014 na waliomaliza mwaka 2014 walipangiwa mwezi wa tano 2015. Lakini mamia ya walimu waliohitimu mwaka 2015 ,hawajaajiriwa,wanaendelea kusota mitaani.Kuchelewa sana kwa ajira za ualimu kumekithiri  kat

SERIKALI INGEANZA KWANZA NA WALIMU

NA RUSTON MSANGI. Taaluma  ya ualimu ni mama na mhimili wa taaluma zote duniani. Hakuna Taaluma au fani isiyotokana na ualimu. Ualimu ndio unaojenga daraja la uhusiano baina ya taaluma zote duniani.Kwamba watu waliopata taaluma au kusomea fani mbalimbali duniani walipikwa na kuivishwa kwenye chungu cha ualimu.  Ualimu ndio unaotengeneza ,wanasheria, wahandisi, wahasibu na hata mwandishi wa habari, wanasiasa. Dhima ya ualimu ni kutoa au kufundisha   maarifa, ujuzi na hekima. Ualimu ni mchakato wa kufundisha maarifa, ujuzi au hekima kutoka kwa mtu moja kwenda kwa mwingine. Mtoaji maarifa au hekima anaitwa mwalimu na mpokeaji ni mwanafunzi. Wanafalsafa wa kale walifanya kazi ya ualimu kwa vitendo na walifanikiwa kuzalisha kizazi chenye hekima, maarifa na ujuzi tele. Waliacha urithi usiochakaa wala kuharibika vizazi na vizazi. Mwanafalsafa Socrates aliyeishi Ugiriki ya kale kati mwaka 469-399 Kabla ya Kristo(B.K) aliishi kwa kutafakari ,kuhoji na kutafuta na kufundisha hekim

MAWAZIRI WA ELIMU WANAVYOKOROGA KWA ZAMU.

➡sasa ni zamu ya Profesa Ndalichako. Anaandika Ruston Msangi. Kila mwanadamu huzaliwa huru. Anapozaliwa haijulikani mara moja atakuja kuwa nani au mwenye taaluma/ fani gani. Lakini kutokana na malezi ya wazazi, mazingira, na jamii inayomzunguka mtoto huanza kutamani kuwa mtu flani hapo baadae. Kutoka ngazi ya jamii, ndoto za mtoto huamia shuleni ambapo ndipo hasa eneo la muhimu katika kujenga misingi ya daktari, Mwalimu, mwanasheria, Mhasibu, Askari, mwanajeshi, mwanahabari nk. wa kizazi kijacho. Uwezo wa mtoto kimasomo Kulingana na fani itakayo hujulikana akiwa shule. Kila mtoto anakuwa na uwezo kwenye eneo Lake Kulingana na kipaji chake. Hivi vyote vinatokana na misingi ya Taifa, sera, mikakati, mipango ya muda mrefu na mazingira rafiki yenye mahitaji yote muhimu ya kujifunzia ndivyo ambavyo humuwezesha mwanafuzi kutimiza ndoto yake. Ndoto ya mwanafunzi ikitimia basi na ndoto ya Taifa itakuwa imetimia kwa kupata wataalamu viwandani na maeneo yote muhimu. Hivi ndivyo amb

SERIKALI INAVYOZIKA NDOTO ZA KUPATA ELIMU BORA

Na Ruston Msangi. Elimu ni muhimu na nguzo kwa watu na taifa lolote duniani. Siri ya mataifa mengi yaliyoendelea kama Marekani, Uingereza, Urusi, Japan,  China, Ufaransa, Ujerumani na mengineyo,Ni elimu bora. Maendeleo ya mataifa hayo yanatokana na kuwekeza katika elimu bora ambayo baadae imewaletea wataalamu wengi,  teknolojia na maendeleo kwa ujumla. Utambulisho mojawapo wa nchi maskini,zinazoendelea kama vile Tanzania, ni elimu duni. Wakati rekodi zinaonesha elimu ndio mhimili wa Maendeleo duniani, Tanzania na nchi nyingine maskini zinaelezwa kuzika elimu kaburini. Mikakati, mipango na utekelezaji wake, vimekuwa vikisusua sana. Inarudisha nyuma ubora wa elimu. Kwa mfano nchini Tanzania kumekuwa na mipango mingi ya kuboresha elimu, japo mipango mingi imeonekana kushindwa. Leo tuangalie MABADILIKO MAKUBWA YA MFUMO WA MTIHANI WA KIDATO CHA PILI. Hivi karibuni Wakuu wa shule mbalimbali nchini wamepokea waraka kutoka kwa Katibu tawala wa mkoa kupitia kwa wakurugenzi