Posts

Showing posts from October, 2016

WOGA UNAVYOWATESA WALIMU!

Image
NA RUSTON MSANGI. Kwa mujibu wa kamusi ya kiswahili sanifu toleo la pili, 2004, Woga ni hali ya kuwa na hofu ya kufikwa na jambo la kutisha au la taabu. Hali ya kutoweza kustahimili vitisho, hofu. Waajiriwa wote ulimwenguni wanapaswa kufanya kazi kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu. Wakiwa wanatimiza wajibu wao na kupata haki zao bila mateso na manyanyaso yoyote ndani na nje ya eneo la kazi. Nchini Tanzania hali iko tofauti sana kwa wafanyakazi wengi, hususani WALIMU, ambayo ni kada pekee yenye watumishi wengi nchini. Kwa muda mrefu sana walimu wamekuwa ni kundi pekee ambalo kila kiongozi wa nchi hii anaona ni sehemu ya kuchukulia umaarufu. Wakuu wa wilaya, wakurugenzi, viongozi wa kata, viongozi wa CCM nk,  Kwa muda mrefu kwa nyakati tofauti wamekuwa wakimtumia Mwalimu kama sehemu ya kujaribia utendaji wao. Manyanyaso, udhalilishaji na ukandamizwaji kwa Walimu sio kwamba walimu wanaupenda na kukubali, bali ni WOGA tu unawasumbua walimu wengi. Matukio mengi ya kud

Mwanafunzi Alivyochochea Hasira za walimu.

➡Siku ya walimu yaingia dosari. NA RUSTON MSANGI. Kulingana na maelezo ya Kamusi ya kiswahili sanifu, toleo la pili, 2004,dosari ni kasoro,walakini.Dosari ni hali ya kutokuwepi kwa ukamilifu wa kitu. Octoba 5 ya kila mwaka ni siku ya walimu duniani. Katika siku hii maalum, Walimu wote ulimwenguni kwa kushirikiana na mashairika pamoja na Wadau wa elimu huadhimisha na kusherekea siku hii kwa namna mbalimbali. Hufanyika matukio kama mikutano, vikao na shughuli nyingi ambapo walimu na Wadau hushiriki. Mafanikio na changamoto Katika kada ya ualimu na mchango wake katika elimu ya taifa fulani hujadiliwa na kuchambuliwa. Aidha,wakati wa siku hii,walimu na wadau wa elimu, hujikita katika mjadala wa  namna ya kutatua kero mbalimbali ili kuleta ufanisi kwenye elimu na taalauma ya ualimu. Walimu hubadilishana uzoefu. Nchini Tanzania, walimu wamekuwa mjadala.Mjadala juu ya walimu unatokana na tukio la kushambuliwa kikatili kwa mwanafunzi anayedaiwa kugoma na kupiga mwalimu wa m

Mwenge unavyoumiza walimu.

Image
    NA RUSTON MSANGI. Mwenge ni kitu mfano wa kikombe chenye mpini mrefu na utambi ambacho huwashwa na kukimbizwa katika kusherekea au kutukuza jambo fulani. (Kamusi ya kiswahili sanifu, toleo la pili 2004). Mwenge huweza kufananishwa na koroboi/kibatari lakini mwenge ni mkubwa kwa umbo. Nchini Tanzania tuna mwenge wa uhuru ambao azimio la kuuwasha lilitangazwa na Mwalimu Julius Kambarage Nyerere mwaka 1959. Kwa mara ya kwanza ulipandishwa katika kilele cha mlima Kilimanjaro usiku wa Desemba 9, 1961. Hii ilikuwa ni siku ambayo Tanganyika ilipata uhuru wake kutoka kwa waingereza. Mwenge huu ukiwa ni ishara ya uhuru, upendo, utu na matumaini. Kila mwaka huwa kuna mbio za Mwenge, ambapo mwenge hutembezwa kila kona ya nchi, ukibeba ujumbe tofautitofauti wa kijamii, kisiasa na kiuchumi. Malengo na ujumbe wa Mwenge huwa mzuri, lakini shida ni katika utekelezaji wake na matumizi ya pesa. Inaelezwa kwamba Mwenge hauna bajeti maalumu inayopangwa bungeni, lakini ni mojawapo

Hitaji la walimu sio bati.

Image
NA RUSTON MSANGI. Kila chama cha wafanyakazi nchini kina jukumu la kusimamia, kulinda, kuboresha maslahi, na kuhakikisha haki za wanachama wake hazivunjwi, wala kukiukwa kwa namna yoyote ile. Majukumu hayo ya chama chochote cha wafanyakazi hayaepukiki kwa kuwa wanachama huwa na utaratibu maalumu wa kuchangia kwa njia ya ada. Michango hii kwa baadhi ya vyama huwa ya lazima hata kama haujajiunga wala kufahamu utaratibu wowote wa namna chama kinavyoendeshwa. Mfano mzuri ni Chama cha Walimu Tanzania CWT, walimu wengi hawajajiunga kwa kuridhia, bali kwa lazima na kuanza kukatwa pesa 2% ya mshahara mara moja. Mojawapo ya dhumuni muhimu la chama cha walimu Tanzania limeelezwa kwenye katiba ya CWT toleo la 2004, katika sehemu ya kwanza, 4 (s)Kuwekeza katika vitega uchumi vitakavyoboresha ustawi wa wanachama ingawa si Chama cha kibiashara. Kwa msingi huu wa kikatiba tungetegemea vitega uchumi vya CWT kunufaisha walimu na si viongozi pekee. Pamoja na makato hayo ya 2% ya mshah