Posts

Showing posts from December, 2016

Lugha za kimakabila zina athari kwenye elimu yetu!

NA RUSTON MSANGI.  Lugha ni mpangilio wa sauti na maneno unaoleta maana ambao hutumiwa na watu wa taifa fulani au kundi fulani kwa ajili ya kuwasiliana. Lugha inayotumiwa rasmi na watu wa taifa fulani huitwa lugha ya taifa na ile inayotumiwa kundi fulani la watu hasa makabila ni lugha za kimakabila.Kuna lugha huitwa lugha mama.Kila mtu mwenye uwezo wa kuzungumza ana lugha  mama. Lugha mama ni ile lugha ambayo mtoto anapozaliwa hukutana nayo na ndiyo lugha ya kwanza kujifunza kuzuizungumza kuitumia kuwasiliana.Pia,inajulikana kama lugha ya kwanza. Kwa mfano, mtoto akizaliwa leo  katika jamii ya watu wanaotumia kiswahili,akajifunza na  kuweza kukitumia kwa mawasiliano,basi hiyo ndiyo lugha yake ya mama. Au mtoto aliyezaliwa leo na kujifunza kuwasiliana kwa lugha ya  kisukuma,  akaweza,hiyo ndiyo lugha mama kwake.Watanzania wengi lugha zao mama ni zile za kimakabila. Katika mfumo wetu wa elimu nchini Tanzania tunazitambua lugha mbili.Kiswahili kinatumika kufundishia elimu