Posts

Showing posts from September, 2016

Ufaulu hauji kwa kufanya kazi kama watumwa!

NA RUSTON MSANGI. Shughuli yoyote ile ya kimaendeleo inapofanyika, hutegemewa kuwa na matokeo chanya. Hadi kufikia matokeo yanayohitajika, njia za aina tofauti tofauti hutumiwa kufikia mafanikio. Ubora au ubaya wa njia itakayotumika inategemeana kwa kiasi kikubwa na uongozi wa wa shughuli au eneo husika. Vivyo hivyo katika mfumo mzima wa elimu nchini Tanzania, shuleni tunapopeleka vijana/wanafunzi wetu kupata maarifa tunatarajia wapate matokeo mazuri na kufaulu mitihani yao. Ili ufaulu unaotarajiwa uweze kupatikana kwa wanafunzi wetu, wasimamizi wa elimu na viongozi wa Shule wanategemewa kuwa na mbinu, maarifa, weledi na ushirikiano wa kutosha kutoka kwa walimu ambao ndiyo watekelezaji wakuu wa sera na mipango ya elimu. Hivyo kukiwa na mipango mizuri kwa ushirikiano, hata matokeo yatakuwa mazuri. Kutokana na umuhimu wa elimu nchini, nalazimika kuzungumzia ufaulu, namna ya kufanikisha na vikwazo vilivyopo kwa wasimamizi hasa mashuleni kama ambavyo kila kukicha yanajitokez

Posho hii ifike hadi kwa walimu

Image
NA RUSTON MSANGI. Kila mfanyakazi anapoajiriwa huwa kuna utaratibu maalumu wa malipo, yaani mshahara kwa mwezi au vyovyote vile kutokana na mkataba wa kazi. Mbali na malipo ya mshahara katika ajira, pia huwa kuna namna tofautitofauti ya kuwapatia fedha ya ziada wafanyakazi wa eneo au taasisi fulani ili kuongeza morali ya ufanyaji kazi, kupunguza makali ya maisha,  kufidia muda wa ziada katika kazi nk. Hii fedha hujulikana kama posho. Posho hii inaweza kutolewa kwa mwezi, siku, saa nk.  Posho huweza kuwa kwa ajili ya chakula, usafiri, malazi,   utendaji au namna yoyote ili itakavyokuwa imepangwa na mwajiri kwa makubaliano maalumu. Watumishi nchini Tanzania katika serikali na mashirika binafsi wanapokea posho kutokana na majukumu Yao. Kwa mfano, madaktari na polisi. Kwa upande wa walimu kwa muda mrefu imekuwa ni tofauti sana kuhusiana na suala la posho, japokuwa mwalimu mbali na jukumu kubwa na muhimu la kufundisha,  hufanya kazi nyingi nyingine akiwa kazini. Kilichon

Bodi ya mikopo kwa hili Hapana

NA RUSTON MSANGI. Mataifa mengi ulimwenguni yaliyoendelea na yanayoendelea, serikali zina  utaratibu maalumu wa kusaidia wanafunzi katika nchi zao kwenye masuala ya Elimu. Utaratibu huu hupelekea kuundwa kwa vyombo na taasisi mbalimbali zinazoshughulikia mikopo hasa ya Elimu ya juu. Vivyo hivyo nchini Tanzania tuna utaratibu wa utoaji wa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu wenye sifa, sifa kuu ikiwa ufaulu na fani husika. Bodi ya mikopo nchini ilianzishwa kwa sheria ya Bunge namba 9, ya mwaka 2004 na Bodi ilianza rasmi mwezi julai, 2005. Moja ya Majukumu muhimu ya bodi ya mikopo yakiwa yafuatayo,- Mosi, Kusimamia mchakato wa Uombaji mikopo/kuwapata wanufaika stahiki wenye kukidhi vigezo baina ya waombaji. Mbili, utoaji wa mikopo. Tatu, Kukusanya mikopo iliyokopeshwa tangu mwaka 1994. Bodi ya mikopo pamoja na mapungufu makubwa iliyokuwa nayo na ambayo inayo,  imekuwa msaada mkubwa kwa familia masikini nchini. Wanufaika ni mashahidi wa hili. Taarifa ya habari ya Se

HUU NI UHAKIKI AU UDHALILISHAJI?

NA RUSTON MSANGI. Serikali ya awamu ya tano tangu iingie madarakani takribani mwaka mmoja uliopita, imekuwa ikiratibu na kutekeleza mengi nchini. Hivyo kuna mfululizo wa matukio mengi yaliyojitoleza. Matukio hayo yapo mazuri, mabaya na zaidi yapo yakushangaza na kustaajabisha machoni na masikioni mwa watanzania. Zoezi la uhakiki wa vyeti ni mojawapo ya mambo yaliyovaliwa njuga na serikali. Leo Naomba nizungumzie zoezi hili linaloendelea la kuhakiki vyeti vya watumishi walipo kazini. Nieleweke kuwa sipingi uhakiki wa vyeti nchini kwa namna mpya ambayo licha ya kushangaza wengi, lakini pia imewaacha wengi na maswali bila majibu. Nikiri kutoka moyoni zoezi la uhakiki likifuata kanuni, sheria, taratibu, utaalamu na ushirikishwaji wa taasisi tofautitofauti, Ni zoezi zuri kwa maslahi ya taifa, LAKINI kinyume na hapo inakuwa fujo na udhalilishaji. KAMA taifa nilitegemea tuwe na mfumo mmoja wa namna ya uhakiki, na pia sio dhambi kutofautiana kwa baadhi ya Halmashauri katika namna y