Posts

Showing posts from July, 2016

UZALENDO WA KWELI HAUNA MIPAKA.

Image
. Na, Emmanuel Chengula, Uzalendo ni hali ya kupenda, kuamini, ama pengne kukihusudu kitu fulani kutoka moyoni bila kuwa na mazingira ya kukulazimisha kufanya hivyo. Uzalendo ni zaidi ya love affection, ni zaidi ya mashart ni zaidi ya shinikizo na una kawaida ya kutenda haki na pengine kutoa uhai wa watu au mtu ili kitu hicho kisalimike. Duniani kote kuna mgawanyiko wa watu wenye baadhi ya dondoo za uzalendo lakini sio wazalendo kama lilivo neno lenyewe lakin pia wachache walihesabika ni wazalendo kama mwl nyerere, Nkwame nkrumah, steve bikko, Nelson Mandela, Marcus Gurvey, Martin Luther Jr, Indra Gandhi n.k. Kwa kawaida uzalendo wa kweli ni ule unaoangalia nchi kwa ujumla pamoja na watu wake japo kuwa kuna watu ambao wameugawa uzalendo na kuegemea kwenye chombo ama kitu kimoja; mfano kuna wazalendo wa vyama vya siasa, dini, serikali tu, bunge tu, mahakama tu, haki za wanyonge tu matajiri hana uzalendo nao, matajiri tu maskini hataki hata kuwasikia, wenye ufahamu mzuri tu,