MAANA HALISI YA USHOGA KATIKA SIASA. Wapendwa wasomaji wa makala zangu kwanza kabisa niaze kwa salamu, shikamoni wakubwa, habari za leo na hamjambo mlio wadogo kwangu. Ni tumaini langu mu wazima huku mkiendelea kushangilia umasikini tulionao. Awali ya yote ningependa kutoa ufafanuzi kidogo juu ya ushoga japo niliwahi kuandika andiko la kufanana na hili mwaka wa jana mwenzi wa kumi na moja, wengi walikimbilia kutukana tu bila kuangalia maudhui ya andiko nilichokiandiko ndicho kinachoendelea hivi sasa inshallah tuachane na hayo. Nisikuchoshe usinichosha"Ushoga"una maana kuu mbili nijuavyo mm na wachache au wengi wetu. Maana ya kwanza ushoga ni tabia ya mwanaume kuingiliwa kinyume cha maumbile na mwanaume mwenzake yaani mwanaume kuingizwa uume na mwanaume mwenzake kwenye tundu la kutolea haja kubwa (kinyesi) . Hali hii humfanya mtu anayeingizwa kujikuta kuhitaji mara kwa mara kutokana na muwasho anaoupata siku chache baada ya tendo hilo chafu na ovu, kwani wadudu/bacteria
KILIMO CHA NYANYA NCHINI TANZANIA Na Goliath Mfalamagoha Wahenga wanasema “kilimo ni uti wa mgongo” ikiwa na maana kilimo ndio nguzo kuu ya maisha ya mwanadamu pia nami sipingani na kauli hii ya wahenga wetu japo kwa miaka hii ya karibuni imekuwa kinyume na kauli mbiu hii ya wahenga.Nami ningependa kuangazia zaidi juu ya kilimo cha nyanya ambalo ni zao kuu aina ya mbogamboga au tunda ,nyanya inalimwa sana mikoa ya iringa ,Morogoro,Arusha,Shinyanga n.k . Mkulima wa nyanya katika kijiji cha Mgama Bwana Raphael Kihongosi, akifurahia zao la nyanya shambani kwake, anasema pamoja na elimu yake aliyoipata ya Iniformation technology (IT) lakini kwake kilimo ndio baba na mama, hajutii kuwa mkulima japo changamoto ni nyingi. Kuna aina kuu mbili za nyanya ambazo ni nyanya ndefu na nyanya fupi hivyo wakulima hulima kutegemea na aina ipi inastawi zaidi katika eneo lao na urahisi wa kuzitunza,japo asilimia kubwa hupendelea nyanya ndefu kwa sababu fupi huhitaji matunzo makubwa sana
NA RUSTON MSANGI. Kila mfanyakazi anapoajiriwa huwa kuna utaratibu maalumu wa malipo, yaani mshahara kwa mwezi au vyovyote vile kutokana na mkataba wa kazi. Mbali na malipo ya mshahara katika ajira, pia huwa kuna namna tofautitofauti ya kuwapatia fedha ya ziada wafanyakazi wa eneo au taasisi fulani ili kuongeza morali ya ufanyaji kazi, kupunguza makali ya maisha, kufidia muda wa ziada katika kazi nk. Hii fedha hujulikana kama posho. Posho hii inaweza kutolewa kwa mwezi, siku, saa nk. Posho huweza kuwa kwa ajili ya chakula, usafiri, malazi, utendaji au namna yoyote ili itakavyokuwa imepangwa na mwajiri kwa makubaliano maalumu. Watumishi nchini Tanzania katika serikali na mashirika binafsi wanapokea posho kutokana na majukumu Yao. Kwa mfano, madaktari na polisi. Kwa upande wa walimu kwa muda mrefu imekuwa ni tofauti sana kuhusiana na suala la posho, japokuwa mwalimu mbali na jukumu kubwa na muhimu la kufundisha, hufanya kazi nyingi nyingine akiwa kazini. Kilichon
Comments
Post a Comment