NA RUSTON MSANGI. Kila mfanyakazi anapoajiriwa huwa kuna utaratibu maalumu wa malipo, yaani mshahara kwa mwezi au vyovyote vile kutokana na mkataba wa kazi. Mbali na malipo ya mshahara katika ajira, pia huwa kuna namna tofautitofauti ya kuwapatia fedha ya ziada wafanyakazi wa eneo au taasisi fulani ili kuongeza morali ya ufanyaji kazi, kupunguza makali ya maisha, kufidia muda wa ziada katika kazi nk. Hii fedha hujulikana kama posho. Posho hii inaweza kutolewa kwa mwezi, siku, saa nk. Posho huweza kuwa kwa ajili ya chakula, usafiri, malazi, utendaji au namna yoyote ili itakavyokuwa imepangwa na mwajiri kwa makubaliano maalumu. Watumishi nchini Tanzania katika serikali na mashirika binafsi wanapokea posho kutokana na majukumu Yao. Kwa mfano, madaktari na polisi. Kwa upande wa walimu kwa muda mrefu imekuwa ni tofauti sana kuhusiana na suala la posho, japokuwa mwalimu mbali na jukumu kubwa na muhimu la kufundisha, hufanya kazi nyingi nyingine akiwa kazini. Kilichon
Comments
Post a Comment