SAMSON MWIGAMBA AJIUZULU NAFASI YAKE YA UKATIBU MKUU ACT - WAZALENDO
Pichani ni mh Mwigamba katibu mkuu wa ACT wazalendo aliyejiuzulu nafasi yake kwa sababu anakwenda masomoni nchini Kenya Katibu mkuu wa chama cha ACT wazalendo Samson Mwigamba ameamua kujiuzulu nafasi yake ya ukatibu mkuu wa chama. Mwigamba anasema kuwa ameamua kuchukua uamuzi huo kwa sababu anakwenda masomoni inchini Kenya. Kamati ya uongozi wa chama chake wameridhia na kupokea maombi ya katibu huyo, zaidi wamempongeza kwa juhudi zake na uwezo wake katika harakati za kukikuza chama hicho cha upinzani nchini Tanzania, Aidha Mwigamba anasema yeye atabaki kuwa mwanachama hai wa chama cha ACT wazalendo na atashirikiana na wanachama wenzake na viongozi kwa ujumla katika kuendeleza harakati za kukitangaza na kukieneza chama chao nchini na amewashukuru viongozi wenzake, wanachama wenzake na wananchi kwa ujumla kwa ushirikiano wao. Kwa mjibu wa kamati ya uongozi machamato wa kupata katibu mwingine utatangazwa wakati wowote ili mtu mwingine aendeleze harakati za kukijenga...